BENKI
ya NMB imefanikisha kufanyika kwa Tamasha maalum la watoto 'Mtoto Day
Out' kwa kuwa mdhamini mkuu wa Tamasha hilo. Tamasha hilo ambalo
limekutanisha watoto wa maeneo mbalimbali ya jijini Dar es Salaam ambapo
pamoja na kufurahi pia wamepata elimu kuhusu umuhimu wa kutunza fedha.
Akizungumza
kuhusu tamasha hilo, Mratibu wa Elimu ya Fedha wa benki ya NMB, Ryoba
Mkono alisema NMB imedhamini tamasha hilo ili watoto wafurahi lakini pia
wapate elimu kuhusu fedha na umuhimu wa kuzitunza.
Baadhi ya watoto wakicheza kwa furaka katika Tamasha maalum la watoto 'Mtoto Day Out' lililodhaminiwa na Benki ya NMB.
Mkono
alisema pamoja na mambo hayo pia NMB ilitoa ofa ya watoto kufunguliwa
akaunti ya Mtoto na Chipukizi akaunti bure kwa watoto waliohuddhuria
tamasha hilo lakini pia kuwapa zawadi za aina mbalimbali ambazo walikuwa
wamewaandalia kwa siku hiyo.
“Sisi kama wadhamini wa
Mtoto Day Out NMB tumewaletea elimu ya fedha na umuhimu wa kuweka akiba
lakini pia kuwafungulia watoto akaunti bure lakini pia imekuwa njia bora
ya kukutana na wazazi maana tumekuwa tukikutana na watoto mashuleni
lakini wazazi hatukutani nao, “Lakini pia sababu NMN inathamini elimu
tumeamua kununua madaftari yenye logo ya NMB, karamu, rula, mabegi,
penseli kwa ajili ya watoto na zawadi zetu zinaandana na elimu,” alisema
Mkono.
Baadhi ya maofisa wa NMB wakigawa zawadi kwa watoto katika Tamasha maalum la watoto 'Mtoto Day Out' lililodhaminiwa na Benki ya NMB.
Kwa upande wa mmoja wa waandaji wa tamasha hilo,
Glory Shayo alisema dhumuni la kuandaa tamasha hilo ni kukutanisha
watoto wafurahi kwani wao huwa hawapati nafasi ya kutoka tofauti na
wazazi hivyo siku hiyo ilikuwa muhimu kwa ajili yao na wao kufurahi kwa
pamoja na kupata elimu ya fedha kutoka NMB.
“Tumeanda
tamasha kwa ajili ya watoto, wazazi tuna out nyingi muda mwingine
tunawapeleka kwenye sehemu za wazazi lakini wanakpata wapi muda wa
kukutana, muda wa kujifunza na kushiriki michezo na wenzao? ni
changamoto ni vema wakipata nafasi ya kukutana na kucheza kwa pamoja na
kupitia NMB tukaandaa hii Mtoto Day Out,” alisema Glory.
Zawadi mbalimbali zikitolewa kwa watoto kutoka Benki ya NMB kwenye Tamasha maalum la watoto 'Mtoto Day Out' lililodhaminiwa na NMB. Baadhi ya watoto wakicheza kwa furaka katika Tamasha maalum la watoto 'Mtoto Day Out' lililodhaminiwa na Benki ya NMB.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...