Benki ya NMB imekuja na huduma yake ijulikanayo kama Trade Finance yenye lengo lakuendana na mabadiliko na kuendeleza Uchumi wa Viwanda nchini.

Trade Finance ni utaratibu wa Benki ambao unamwezesha Mteja kama Mkandarasi, Wazalishaji na Wasambazaji kupata bidhaa na huduma za Kibiashara ndani na nje ya nchi.

Akizungumza na Waandishi wa Habari katika Warsha fupi iliyoandaliwa na Benki hiyo, Mkurugenzi Mtendaji - NMB, Bi. Ineke Bussemaker amesema kuwa huduma hiyo inahusika na Manunuzi pamoja na kuleta vifaa mbalimbali kutoka nje ya nchi, Usafirishaji wa Vifaa na bidhaa mbalimbali.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo hiko cha Trade Finance, Bi. Linda Mtango Teggisa amesema kuwa Kitengo hiko kinahusika pia katika udhamini kwa Mteja endapo atashindwa kulipia huduma hiyo.

Pia amesema kuwa Benki italazimika kufanya mapitio ya taarifa za Mteja pale inapotokea Mteja huyo kuhitaji dhamana.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Bi. Ineke Bussemaker akizungumza katika Warsha iliyoandaliwa na Benki hiyo katika kuhusu huduma ya Trade Finance.
Mkuu wa Kitengo cha Trade Finance, Bi. Linda Mtango Teggisa akizungumzia juu ya Kitengo hiko kinahusika pia katika udhamini kwa Mteja endapo atashindwa kulipia huduma hiyo.
Mmoja wa Wataalamu wa huduma hiyo ya Trade Finance katika Benki ya NMB akitoa ufafanuzi kuhusu huduma hiyo inavyofanya kazi kwa Wateja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...