DROO maalum ya kuwania Sh Milioni 10, iliyoandaliwa na waandaaji wa mchezo wa kubahatisha wa Biko, imeenda kwa kijana mwenye miaka 25, Said Juma, mkazi wa Mwanza, ikitolewa katika tamasha la burudani la Komaa Concert la EFM Radio, lililofanyika katika Uwanja wa CCM Kirumba, jijini hapa jana.

Katika tamasha hilo, wasanii mbalimbali wa jijini Mwanza na Dar es Salaam, walipata nafasi ya kutoa burudani kwa mashabiki wao, huku likinogeshwa na Milioni 10 za Biko maalum kwa wakazi wa Mwanza pekee.

Akizungumza katika droo hiyo ndani ya Uwanja wa CCM Kirumba, Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, alisema mshindi huyo alipatikana kwa kupigiwa simu kama wanavyopatikana wengine waliowahi kuvuna mamilioni kutoka kwenye bahati nasibu yao inayochezeshwa kwa njia ya ujumbe wa maandishi kwa kupitia mitandao ya simu za Tigo Pesa, Airtel Money na M-Pesa.

Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven kushoto mwenye kipaza sauti, akimtangaza Said Juma kulia, aliyefanikiwa kunyakua jumla ya Sh Milioni 10 za Biko zilizotolewa maalum kwa ajili ya Tamasha la Komaa Concert lililoandaliwa na EFM Radio Jumamosi iliyopita na kufanyika katika Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza.

Shabiki wa muziki wa kizazi kipya jijini Mwanza ambaye jina lake halikupatikana mara moja akifuatilia onyesho la Komaa Concert lililoandaliwa na EFM Radio na kudhaminiwa na Bahati Nasibu ya Biko, ambapo pia alitafutwa mshindi wa Sh Milioni 10 wa Biko na Said Juma mkazi wa jijini Mwanza kuibuka kwenye droo hiyo maalum.

Baadhi ya mashabiki wa muziki wa jijini Mwanza, wakiwa katika shangwe kubwa huku mmoja wao akiwa amevaa tshirt ya Biko wadhamini wa tamasha la burudani la Komaa Concert lililoandaliwa na EFM Radio kwa udhamini wa waendeshaji wa bahati nasibu ya Biko, ambapo pia ilimtangazaa mshindi wake maalum kwa ajili ya tamasha hilo ambaye ni Said Juma wa jijini Mwanza aliyezoa Sh Milioni 10 za Biko Tamasha hilo lilifanyika jana Jumamosi na kufanyika katika Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza.

Alisema kuwa watu waliocheza kwa kufanya miamala kwenye simu zao kuanzia Sh 1000 na kuendelea walichezeshwa kwenye droo moja iliyompa ushindi Juma, huku wakicheza kwa kutumia namba ya kampuni ya 505050 na ile ya kumbukumbu ya 2456.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...