Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini Mh.Christina Mndeme leo amefanya ukaguzi kwenye vituo vya mafuta ili kuona kama wafanyabiashara ya kuuza mafuta wanafuata sheria na taratibu za utoaji risiti na ulipaji kodi kwa kufunga mashine sahihi ya utoaji risiti iliyofungwa moja kwa moja kwenye pampu au mita ya mafuta. 

Katika ZIARA hiyo Kati ya vituo 9 alivyovitembelea amegundua kituo kimoja tu ndiyo kinafuata sheria na kuchukua hatua ya kuvifungia vituo nane (08).

Kazi hiyo imefanyika kwa kushirikiana na maafisa wa TRA Dodoma Mjini. Tunatekeleza kwa Hapa Kazi Tu, Lipa kodi kwa Maendeleo ya Taifa letu.

Pichani kushoto ni  Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini Mh.Christina Mndeme akishirikiana na Ofisa wa TRA kukifungia moja ya kituo cha mafuta mkoani humo kilichobainika kutofuata sheria na taratibu za utoaji risiti na ulipaji kodi kwa kufunga mashine sahihi ya utoaji risiti iliyofungwa moja kwa moja kwenye pampu au mita ya mafuta.
Wasimamizi wa kituo wakipewa maelekezo baada ya kituo chao cha mafuta kufungiwa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...