Mkuu
wa Wilaya ya Dodoma mjini Mh.Christina Mndeme leo amefanya ukaguzi
kwenye vituo vya mafuta ili kuona kama wafanyabiashara ya kuuza mafuta
wanafuata sheria na taratibu za utoaji risiti na ulipaji kodi kwa
kufunga mashine sahihi ya utoaji risiti iliyofungwa moja kwa moja kwenye
pampu au mita ya mafuta.
Katika
ZIARA hiyo Kati ya vituo 9 alivyovitembelea amegundua kituo kimoja tu
ndiyo kinafuata sheria na kuchukua hatua ya kuvifungia vituo nane (08).
Kazi hiyo imefanyika kwa kushirikiana na maafisa wa TRA Dodoma Mjini. Tunatekeleza kwa Hapa Kazi Tu, Lipa kodi kwa Maendeleo ya Taifa letu.
Pichani kushoto ni
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini Mh.Christina Mndeme akishirikiana na
Ofisa wa TRA kukifungia moja ya kituo cha mafuta mkoani humo
kilichobainika kutofuata sheria na taratibu za utoaji risiti na ulipaji
kodi kwa
kufunga mashine sahihi ya utoaji risiti iliyofungwa moja kwa moja kwenye
pampu au mita ya mafuta.
Wasimamizi wa kituo wakipewa maelekezo baada ya kituo chao cha mafuta kufungiwa
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...