Naibu
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh.
Dk.Hamisi Kigwangalla ameendelea na ziara yake ya kikazi ya kukagua
huduma za Afya ‘Imarisha Afya’ katika Zahanati, Vituo vya Afya na
Hospitali mbalimbali kwenye mikoa ya Rukwa, Katavi pamoja na Tabora.
Akiwa
katika mkoa wa Rukwa, Dk. Kigwangalla aliweza kutembelea Hospitali ya
Sumbawanga ambayp ni ya Mkoa wa Rukwa na kujionea mambo mbalimbali huku
akiwapongeza kwa namna walivyoboresha huduma zao ikiwemo ile ya Maabara,
Chumba cha upasuaji na huduma zingine ambapo aliwaagiza kuhakikisha
wanakuwa na hakiba ya kutosha ya damu salama kwa ajili ya dharura kwa
wagonjwa wa ukanda huo.
Mbali
na Hospitali ya Mkoa wa Rukwa, pia aliweza kutembelea kituo ca Laela
ambapo pia mbali ya kujionea utendaji kazi wa kituo hicho alipongeza
juhudi za Mbunge wa jimbo la Kwera, Mh. Ignas Alloyce Malocha kwa
kushirikiana na wananchi wake katika masuala ya huduma za Afya.
Ziara hiyo katika
mkoa wa Rukwa, aliweza kumalizia katika Kituo cha Afya Wampembe
kilichopo Wilayani Nkasi ambapo alijionea shughuli mbalimbali ikiwemo
huduma za Upasuaji hata hivyo aliutaka uongozi wa kituo hicho ambacho
kipo mwambao wa Ziwa Tanganyika kuhakikisha wanakamilisha mifum ya maji
safi na salama ndani ya kituo pamoja na kuboresha huduma za Maabara na
usafi kwa ajumla.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akikagua Maabara ya Mkoa wa Rukwa
Naibu
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh.
Dk.Hamisi Kigwangalla akikaguachumba cha upasuaji Hospitali ya Mkoa wa
Rukwa
Naibu
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh.
Dk.Hamisi Kigwangalla akielekea kukagua Maabara ya Kituo cha Afya Laela
Mkoa wa Rukwa
Jengo linaloendelea kujengwa kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya ya Uyui.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...