Kamati ya utendaji ya klabu ya Simba iiliyokutana jana jioni kwenye moja ya kumbi za mikutano za Hoteli ya Serena iliyopo hapa jijini Dar es salaam,imemteua Dr Arnold Kashembe kuwa katibu Mkuu mpya wa klabu. 

Msomi huyo mwenye shahada ya Uzamivu na aliyekuwa Mhadhiri kwenye vyuo mbalimbali barani Ulaya, uteuzi wake unaanza mara moja. 

Pia kamati hyo imepanga kufanya Mkutano wake mkuu wa kawaida tarehe 13-8-2017, huku pia ikitarajiwa kufanya Mkutano Mkuu utakaojadili mabadiliko ya katiba tarehe 20-8-2017.

Mikutano hyo imeitishwa kwa kuzingatia takwa la kikatiba la klabu,linalotaka notisi ya kuitishwa mikutano hiyo,ifanywe sio chini ya siku Thelathini kabla ya mikutano yenyewe. 

Klabu inatarajia kutoa taarifa zaidi juu ya maandalizi na taratibu za mikutano hiyo katika Siku chache zijazo na inaendelea kuwaomba Wanachama na Washabiki wake muendelee kuwa na utulivu,hususan kipindi hiki ambacho baadhi ya viongozi wetu wakiwa kwenye Shauri lao,liliopo Mahakamani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...