Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dk Aloyce Nzuki akizungumza na baadhi ya watumishi wa wizara hiyo alipotembelea banda la Wizara hiyo Maonyesho ya Maonyesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa, yaliyoanza Juni 28 - Julai 8, 2017 ambapo kwa mwaka huu yameongezewa siku tano zaidi na kutarajiwa kumalizika Julai 13, 2017, yaliyozinduliwa rasmi leo jijini Dar es salaam.
Afisa Uhusiano wa Bodi ya Utalii Tanzania, Geofrey Tengeneza, akiwa katika mahojiano na Mwandishi wa kituo cha Radio cha Clouds Fm Power Breakfast ndani ya banda hilo akizungumzia juu ya utalii wa ndani
Sehemu ya Watanzania waliotembelea banda Maliasili na kujionea wanyama mbalimbali ndani ya Zoo ndogo.
Simba jike na Dume wakionekana ndani ya Zoo iliyopo ndani ya banda la Wizara ya maliasili ndani ya Maonyesho ya Sabasaba
Mbega wakiwa ndani ya Zoo iliyopo ndani ya banda la Wizara ya maliasili katika Maonyesho ya Sabasaba.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...