Na Benny Mwaipaja, WFM 
WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, amewapongeza Watanzania nchini kote kwa mwitikio wao mkubwa wa kulipa kodi mbalimbali ikiwemo ya majengo kwa hiari, hatua ambayo itaiongezea Serikali uwezo wa kuwahudumia kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.
Dkt. Mpango ametoa pongezi hizo alipotembelea maonesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea katika uwanja wa maonesho ya Biashara wa Mwal. J. K. Nyerere, Barabara ya Kilwa Jijini Dar es Salaam.
Ametoa wito kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kulipa kodi kwa maendeleo ya Taifa pamoja na kuwahimiza wananchi kudai risiti wanapofanya manunuzi halkadhalika wafanyabiashara kutoa risiti wanapouza bidhaa kwa mujibu wa sheria za nchi.
Baadhi ya wananchi waliofurika kulipa kodi mbalimbali hususan za majengo katika viwanja hivyo vya Sabasaba, wameeleza kuwa mwitikio na hamasa kubwa waliyonayo ya kulipa kodi inatokana na imani yao kwa Serikali ya Awamu ya Tano jinsi inavyosimamia maendeleo ya nchi kwa umakini mkubwa.
Kwa upande wake Meneja wa Huduma kwa Mlipakodi Bi. Honesta Nduguru, amewataka Watanzania popote walipo kutumia muda mfupi wa nyongeza uliobaki kulipa kodi badala ya kusubiri dakika za lala salama.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango akisikiliza maelezo toka kwa Bi. Honesta Ndunguru, Meneja Huduma kwa Mlipakodi, wa TRA alipotembelea maonesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea katika uwanja wa maonesho ya Biashara wa Mwal. J. K. Nyerere, Barabara ya Kilwa Jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...