Na Karama Kenyunko, Globu ya jamii.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeambiwa Mfanyabiashara  Yusufali Manji (41) bado anaumwa na yuko kwenye matibabu katika hospitali ya gereza la mahabusu la Keko jijini Dar es salam.
Wakili wa Serikali Mwandamizi Bw. Nassoro Katuga amedai hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Mhe. Huruma Shaidi wakati kesi hiyo ilikuja kwa kutajwa.
Amedai kuwa, kesi hiyo leo ilikuja kwa kutajwa lakini Upelelezi bado haujakamilika na kesi hiyo itatajwa tena Agosti 4, mwaka huu.

Katika kesi hiyo Manji na wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba chini ya sheria ya uhujumu uchumi na usalama wa Taifa.
Katika Mashtaka hayo, wanadaiwa kukutwa na vitambaa vinavyotengeneza sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania vyenye thamani ya zaidi ya milioni 195.5 na mihuri ya JWTZ na magari ya serikali kinyume cha sheria.
Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Meneja Rasilimali watu wa kampuni ya Quality Group Deogratius Kisinda(28), mtunza stoo Abdallah Sangey(46) na Thobias Fwere (43) mkazi wa Chanika.


Mfanyabiashara  Yusufali Manji

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...