Hatimaye Mwenyekiti wa Jumuiya ya
Wazazi Tanzania, Alhaj Abdallah Bulembo ametii shinikizo lililokuwa
likitolewa na Wazee, viongozi na wanachama wa Jumuiya hiyo kumuomba
agombea tena nafasi yake.
Hayo yametimia kufuatia Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Alhaji Bulembo kuchukua fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea nafasi hiyo, katika Ofisi za Jumuiya ya Wazazi mkoa wa Dodoma leo mchana, huku akifanya tukio hilo kimyakimya tofauti na ilivyozoeleka ambapo baadhi ya wawania uongozi husindikizwa na wapambe na waandishi wa habari.
Licha ya kwenda kimyakimya, lakini taarifa zilizopatikana mjini hapa, zimesema kwamba alifika kwenye Ofisi za hizo za Wazazi mkoa wa Dodoma mda wa saa nane mchana akijiedesha kwa gari namba T888 DFB aina Toyota Land Cruser lenye vioo vya giza, na kukabidhiwa fomu hizo na Mwenyekiti wa Jumuia wa mkoa Gama Juma.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania, Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Alhaj Abdallah Bulembo akikabidhiwa fomu ya na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo mkoa wa Dodoma, Gama Juma, leo.
Hehe sande kwa Kazi mzuri pia tembelea blog yangu genius funs media
ReplyDelete