Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo amefurahishwa na maendeleo ya ujenzi wa shule ya wavulana ya kidato cha tano na sita ya Ihungo ambayo majengo yake yalibomoka kutokana na tetemeko la ardhi lililotokea mwaka Jana.

Kutokana na kubomoka kwa majengo hayo, Serikali iliamua kuijenga upya kwa kutumia wakala wa majengo Tanzania (TBA). Akiwa katika ziara ya kukagua miradi mbalimbali mkoani Kagera, Jafo alitembelea shuleni hapo kukagua ujenzi wake.

Naibu Waziri Jafo aliwapongeza wakandarasi kwa kazi nzuri wanayoendelea kuifanya ambapo kazi hiyo inatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Agosti. Akizungumza na wananchi waliokuwepo katika eneo hilo, Jafo alisema serikali imeamua kuijenga sekondari hiyo kisasa zaidi. Alisema sekondari hiyo inatarajiwa kuwa sekondari ya mfano ndani ya Tanzania kwa kuwa na majengo ya kisasa zaidi kuliko sekondari zote hapa nchini.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akifanya ukaguzi wa miundombinu inayojengwa katika Shule ya Sekondari Ihungo. 
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akiwa katika ukaguzi wa ujenzi wa madarasa na mabweni katika Shule ya Sekondari Ihungo. 
Jengo la bweni linalojengwa katika shule ya Sekondari Ihungo. 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...