Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo amewataka wananchi wa wilaya ya Ukerewe kutunza miradi ya Maji kwa kuwa serikali inaigharamia kwa fedha nyingi.

Jafo aliyasema hayo alipotembelea mradi mkubwa wa maji wa Kazilamkanda ambao utahudumia vijiji vipatavyo 13 wilayani humo.

Amesema serikali inafanya jitihada za kuwatatulia wananchi wake kero mbalimbali ikiwemo ya upatikanaji wa huduma ya maji, hivyo ni vyema wakatunza miundombinu ya miradi hiyo ili iweze kudumu kwa muda mrefu.

Akikagua mradi huo, Jafo alimpongeza Mkandarasi aliye jenga chanzo na tanki la kuhifadhia maji la lita 680,000 ambaye ni Lutare Make Enginnering Ltd kwa kazi nzuri.

Amesisitiza kukamilishwa kwa usambazaji wa Maji katika vijiji vyote 13 kabla  ya Disemba 30 mwaka huu.

Naibu Waziri huyo amesisitiza kulazwa mabomba yaliyo na ubora ili kuepusha kupasuka kwa mabomba endapo mabomba hayo yatakuwa hayana viwango na kusababisha hasara kubwa kwa wananchi na halmashauri baada ya kukabidhiwa mradi husika.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akizungumza na wananchi wa kijiji cha Rutala wilayani Ukerewe mkoani Mwanza juu ya utunzaji wa miradi ya maji.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akipata taarifa kuhusu miradi ya maji wilayani Ukerewe.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akifanya ukaguzi wa tenki la maji.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akifanya ukaguzi wa mashine za kusukumia maji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...