Na Agness Moshi-MAELEZO
Taasisi
ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imekua mkombozi kwa wagonjwa wa moyo
Afrika Mashariki kufuatia kupungua kwa gharama za matibabu ukilinganisha
na ilivyokua hapo awali.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mbunge wa jimbo la Dokolo nchini Uganda Bi.Cecilia Barbara alipotembelea taasisi hiyo ili kuona na kujifunza jinsi Serikali ya Tanzania inavyotoa huduma za Afya kwa wananchi wake .
Bi.Cecilia amesema taasisi hii ni msaada mkubwa kwa Afrika Mashariki kwasababu itasaidia kupunguza idadi ya wagonjwa wa moyo wanaopelekwa nchini India au Afrika Kusini kwa matibabu kama ilivyo awali baadala yake watatibiwa Tanzania au nchini kwao.
“Tunahitaji kubadilishana mawazo kama wana Afrika Mashariki, kwasababu kwa kuja hapa tumegundua tunavifaa na uwezo wa kupunguza gharama za matibabu ya moyo“ Alisema Bi.Cecilia.
Bi Cecilia amesema kutokana na ubora huduma zinazotolewa na taasisi hii tangu kuanzishwa kwake serikali ya Uganda imekubali kuja kutembelea Tanzania ili kujifunza na kuanzisha mradi kama huu.
“Hatukujua kama Tanzania kuna mradi mkubwa kama huu na unaofanya kazi nzuri lakini kwa kuja tumejua na tunategemea kuanzisha mradi kama huu japo itatuchukua muda kufikia hatua iliyofikiwa na Tanzania”aliongeza Bi.Cecilia .
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mbunge wa jimbo la Dokolo nchini Uganda Bi.Cecilia Barbara alipotembelea taasisi hiyo ili kuona na kujifunza jinsi Serikali ya Tanzania inavyotoa huduma za Afya kwa wananchi wake .
Bi.Cecilia amesema taasisi hii ni msaada mkubwa kwa Afrika Mashariki kwasababu itasaidia kupunguza idadi ya wagonjwa wa moyo wanaopelekwa nchini India au Afrika Kusini kwa matibabu kama ilivyo awali baadala yake watatibiwa Tanzania au nchini kwao.
“Tunahitaji kubadilishana mawazo kama wana Afrika Mashariki, kwasababu kwa kuja hapa tumegundua tunavifaa na uwezo wa kupunguza gharama za matibabu ya moyo“ Alisema Bi.Cecilia.
Bi Cecilia amesema kutokana na ubora huduma zinazotolewa na taasisi hii tangu kuanzishwa kwake serikali ya Uganda imekubali kuja kutembelea Tanzania ili kujifunza na kuanzisha mradi kama huu.
“Hatukujua kama Tanzania kuna mradi mkubwa kama huu na unaofanya kazi nzuri lakini kwa kuja tumejua na tunategemea kuanzisha mradi kama huu japo itatuchukua muda kufikia hatua iliyofikiwa na Tanzania”aliongeza Bi.Cecilia .
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru akizungumza na ujumbe kutoka JICA. Ujumbe huo umetembelea wagonjwa pamoja na miradi mbalimbali ya kuboresha huduma za afya katika hospitali hiyo leo.
Wageni kutoka JICA wakiwa katika ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru. Kutoka kushoto ni Ofisa wa Hospitali Kuu ya Shonan Kamakura, Emiko Shiono, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JICA Idara ya Afrika, Komori Masakatsu, Mwakilishi wa Afrika nchini Japan, Milanga Mwanatambwe na Meneja wa Tiba, Injinia Katsumasa Shirai.
Ofisa Mipango, Catherine Shirima (kulia) wa JICA na Yamae Mikuni kutoka Japan wakiwa kwenye mkutano huo leo.
Wageni hao pamoja na wenyeji wakiwa katika wodi ya wagonjwa Muhimbili leo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...