Mkurugenzi Msaidizi wa
TEHAMA wa Mahakama ya Tanzania, Machumu Essaba akimuelezea Kaimu Jaji Mkuu wa
Tanzania Mhe. Prof.Ibrahim Hamis Juma kuhusu Mfumo wa Takwimu za Mahakama
(JSDS)alipotembelea Banda la Mahakama hivi karibuni katika Maonesho ya 41 ya
Biashara ya Kimataifa katika viwanja vya Sabasaba.
Kaimu Jaji Mkuu wa
Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akiwa katika picha ya pamoja na baadhi
ya Majaji, watumishi wa Mahakama pamoja na watumishi kutoka Taasisi ambazo ni
wadau wa Mahakamawanaoshiriki kwenye Maenesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa
katika viwanja vya Sabasaba.
Kaimu Jaji Mkuu wa
Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akipata maelezo kuhusu utengenezaji wa
samani za nyumbani na maofisini alipotembelea banda la Maonesho la Jeshi la
Kujenga Taifa (JKT) kwenye Maonesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelesa
jijini Dar es salaam.
Kaimu Jaji Mkuu wa
Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akitembelea sehemu mbalimbali katika viwanja vya Mwalimu
Julius Nyerere kwenye Maonesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa katika viwanja
vya Sabasaba jijini Dar es salaam. Aliyefuatana naye ni Kaimu Mkurugenzi wa
Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara ya Tanzania (TANTRADE), Bw. Edwin Rutageruka.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...