Na Bashir
Yakub
1.UKOMO WA
HAKI.
Hakuna haki isiyo
na ukomo wa muda
unapokuwa unaidai. Huwezi kudai
haki muda wowote
unaotaka wewe. Ni lazima
udai haki ndani
ya muda.Na ni
ule muda tu uliowekwa na
sheria. Ipo sheria rasmi
inayoeleza muda wa
kudai haki mbalimbali.
Inaitwa Sheria ya Ukomo
wa Muda , Sura
ya 89. Katika
sheria hiyo hapajaelezwa tu ukomo
wa kudai haki
katika masuala ya ardhi
bali pia katika
masuala mengine yote
ya haki unazoweza
kudai.
Ndani ya Sheria
ya Ukomo wa
Muda kumeelezwa ukomo wa
kudai haki iliyotokana
na masuala ya
mikataba na makubaliano, ukomo wa
kudai haki katika
masuala ya udhalilishaji, ukomo wa rufaa, ukomo wa
haki katika masuala
ya bima, madai ya fedha,
rehani za mikopo, na mambo mengine
mengi.
2. HUJAPITWA
NA MDA BADO UNAWEZA
KUIDAI ARDHI YAKO.
Wako watu huko
nyuma walidhulumiwa ardhi
muda mrefu na
sasa wamekata tamaa.
Wamekata tamaa kutokana na
kuona ni mda mrefu
umepita tangu haki
hiyo iporwe na
sasa wanadhani kuwa
hawawezi tena kudai
haki hiyo.
Wako watu
wamedhulumiwa ardhi katika
masuala ya mirathi,
katika masuala ya
mikopo, katika masuala
ya mikataba na
makubaliano, katika masuala
ya ndoa na
machumo ya mali za
ndoa, katika masuala ya
uvamizi, katika masuala ya
kuharibu mipaka n.k. Na
ardhi hapa tunazungumzia
mashamba, viwanja na
nyumba. Hivi kwa pamoja
ndivyo huitwa ardhi.
Basi yafaa ujue
kuwa kama wewe ni
kati ya waathirika
wa jambo hili
basi bado unayo haki
ya kudai ardhi
yako madhali muda
huo haujakupita. Haki
yako inaishi mpaka
miaka 12 na
itakufa baada ya muda
huo. Kama imepita
miaka sita, mitano,
nane, kumi, n.k.
bado muda wako
wa kudai na
kurudishiwa ardhi upo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...