Na Karama Kenyunko, Globu ya Jamii. 

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imewaamuru Magereza kumpeleka mshitakiwa Harbinder Singh Sethi katika hospitali ya taifa ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu. 

Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi amesema hayo leo, baada ya mshtakiwa Sethi kuieleza mahakama kuwa, anaumwa.

Hakimu Shaidi amesema,suala la afya ya mshitakiwa ni la msingi hivyo mamlaka zinazohusika zihakikishe mshitakiwa anapata matibabu na tarehe ijayo watoe taarifa kama amri imetekelezwa au la.

Kabla ya kutolewa kwa amri hiyo, mshtakia Seth amedai kuwa hali yake ni mbaya kwani aliongea  na magereza ili aweze kupata matibabu toka kwa daktari wake lakini alipelekwa Hospitali ya Amana.

Sethi amedi kutokana na maradhi yake ya uvimbe tumboni kuhitaji mtaalamu, alishindwa kupata matibabu katika hospitali ya Amana.

Mwendesha Mashitaka kutoka  Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Vital Peter alidai suala la ugonjwa ni la kitaalamu ambalo linahitaji kuthibitishwa ili kujiridhisha licha ya mshitakiwa kujieleza, hakuna nyaraka zinazounga mkono hoja zake kutoka kwa mtaalamu zinazoelezea hali yake.

Alidai kutibiwa ni haki ya mshitakiwa kwa kuwa wapo wataalamu katika hospitali  ya Muhimbili na magereza.

Hata hivyo, alidai upelelezi wa shairi hilo haujakamilika na kuomba tarehe kwa ajili ya kutajwa.

Sethi ambaye pia ni Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Power African Power (T) Limited (PAP), anashtakiwa na mwenzake,  James Rugemarila ambaye ni Mkurugenzi wa VIP Engineering na mmiliki mwenza wa zamani wa Kampuni ya Kufua Umeme ya Independent Power Tanzania Ltd (IPTL).

Wote kwa pamoja wanakabiliwa na mashitaka  12 ya  uhujumu uchumi  kwa kuisababishia serikali hasara ya dola za Marekani milioni 22. 1 na Sh bilioni 309.

Hakimu Shaidi aliahirisha kesi hiyo hadi Agosti 3 mwaka huu kwa ajili ya kutajwa na kuangalia upelelezi umefikia wapi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...