Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli leo Ijumaa Julai 07, 2017 amekutana na wazee wasiojiweza wa Wilaya ya Chato na kutoa misaada mbalimbali ya vyakula kwa lengo la kuwapunguzia changamoto zinazowakabili.
Mama
Janeth Magufuli amekabidhi msaada huo kwa wazee zaidi ya 400 kutoka kata 23 za
Wilaya ya Chato mkoani Geita.
Akizungumza
wakati wa utoaji wa msaada huo kwa wazee hao wa Chato Mke wa Rais Mama Janeth
Magufuli ameitaka jamii,watu binafsi,wadau wa maendeleo na taasisi mbalimbali
kushirikiana kwa pamoja katika kuwasaidia wazee hapa nchini.
Mama
Janeth amezitaja baadhi ya changamoto zinazowakabili wazee hao kuwa ni pamoja
na vyakula,madawa na hata upendo na kuthaminiwa.
“Tunawaomba jamani mnaokaa na
wazee muoneshe upendo,muwasaidie pale wanapohitaji msaada,kama wewe una nguvu
basi msaidie hata kuchota maji na kukata kuni kwani hizo ndo Baraka zenyewe”
Kwa
upande wao wazee hao wamemshukuru mke huyo wa Rais kwa moyo wake wa kujitolea
hususani katika kuwasaidia wazee na wasiojiweza huku wakiiomba serikali kuangalia
namna ya kupunguza changamoto zinazowakabili wazee.
Awali
akisoma risala kwa niaba ya wazee hao mbele ya Mke wa Rais Mama Janeth
Magufuli, Afisa Maendeleo wa Jamii Lidiana Kasheku amemueleza Mama Janeth namna
Halmashauri hiyo ilivyojipanga kutatua kero za wazee hao ikiwa ni pamoja na
kuanzisha Baraza la Wazee litakalosaidia kubaini changamoto na aina ya msaada
wanaouhitaji sambamba na kutoa kipaumbele kwa wazee katika huduma mbalimbali
ikiwa ni pamoja na suala la matibabu kwa wazee.
Mama
Janeth Magufuli amekabidhi vitu mbalimbali ikiwa ni pamoja na Mchele, Unga wa
Mahindi,Mafuta ya Kula, Sabuni za kufulia na Maharage.
Wilaya
ya Chato mkoani Geita ina vijini 115 vyenye wazee zaidi ya 18,000 ikiwa ni sawa
na asilimia 5 ya wazee wote nchini barani Afrika.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwakabidhi kwa pamoja mafuta waakilishi wa Wazee kutoka kata ya Kasenga AnatoryBisate (64) kulia pamoja na Bi. Winfrida Lawrent(65) kushoto mara baada ya kuzungumza na wazee 400 katika Ukumbi wa Mshikamano SACCOS Chato mkoani Geita.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiimba pamoja na wanakwaya wa Mwagazege mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa Mshikamano SACCOS Chato mkoani Geita.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akizungumza na Wazee wasiojiweza zaidi ya 400 kutoka Wilaya ya Chato katika Ukumbi wa Mshikamano Saccos.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...