Katika kuunga juhudi za Serikali ya awamu ya tano ya kuleta maendeleo kwa wananchi kampuni ya magari ya Mantrack Tanzania jana imeendesha warsha fupi yenye lengo la kutambulisha vifaa na teknolojia mpya itakayoongeza ufanisi wa kazi hasa katika sekta ya ujenzi.

Akizungumza na waandishi wa habari, mwakilishi wa kampuni ya Mantrack Tanzania alisema kuwa wameleta vifaa vipya vitakavyoendana na kasi ya maendeleo ya Serikali ya awamu ya tano ya kuhakikisha Tanzania mpya inajengwa na uchumi bora na yenye miundombinu bora.

“Vifaa hivi ni imara na vinatumia teknolojia mpya na ya kisasa inayosaidia utendakaji wa shughuli za ujenzi kuwa rahisi. Tumeamua kuja na kasi ya serikali mpya ya kutenda vitu kwa urahisi na kwa ufanisi wa hali ya juu”.

Tuna wakaribisha wadau wa ujenzi wafike kujionea wenye tunachosema. Alisema. Warsha hiyo imefanyika katika karakana ya Mantrack Tanzania iliyopo karibu na jengo la Quality Plaza barabara ya Nyerere na ilihudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka makampuni mbalimbali ya ujenzi hapa nchini waliofika kushuhudia vifaa hivyo vinavyofanya kazi.
Mwakilishi wa ManTrack Tanzania akitoa maelezo mbalimbali kwa wadau juu ya teknolojia mpya na bidhaa zao mbalimbali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...