NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
WAAJIRI na wafanyakazi wamejitokeza
kwa wingi kupata elimu kuhusu kazi za Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF),
kwenye banda la Mfuko huo lililoko kwenye hema kubwa la Jakaya Kikwete kwenye
viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam
kunakofanyika maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam.
Maonesho hayo ya kila mwaka huwaleta
pamoja wafanyabiashara ya makampuni makubwa ya kimataifa kutoka nje na dnani ya
nchi, lakini pia kunakuwepo na mkusanyiko mkubwa wa wafanyakazi wa umma na
binafsi wanaotoa huduma mbalimbali kwa watu wanofika kutembeela maonesho hayo.
Mfuko wa Fidia kwa wWafanyakazi,
(WCF) imetumia fursa hiyo kutoa elimu kwa waajiri na wafanyakazi ambao walifika
kwenye banda la Mfuko huo na kupatiwa maelezo ya kina kuhusu kazi za Mfuko
kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wake Bw. Masha Mshomba, wakurugenzi na wakuu wa
idara pia.
“WCF ni Mfuko wa Hifadhi ya Jamii
ulioanzishwa kwa mujibu wa sheria namba 5 ya Fidia kwa Wafanyakazi kifungu
namba 263 ya mwaka 2015.” Bw. Mshomba aliyasema hayo akiwa kwenye banda hilo
ambapo waajiri na wafanyakazi walifika kupata elimu zaidi ya kuhusu Mfuko huo.
Bw.
Mshomba aliendelea kufafanua
kuwa, kwa mujibu wa sheria iliyoanzasha Mfuko huo, tofauti na Mifuko
mingine ya Hifadhio ya Jamii, ambapo mwajiri na mfanyakazi hutoa
michango ya kila mwezi, kwa upande wa WCF, ni mwajiri pekee ndiye
anawajipika kumchangia mfanyakazi wake kila mwezi na mfanyakazi
hawajibiki kutoa mchango wowote.
Aidha Bw. Mshomba alieleza kuwa, dhumuni kuu la kuanzishwa kwa Mfuko huo ni kutoa Mafao ya kutosha na stahili kwa Mfanyakazi aliyepatwa na maradhi au majeraha yaliyotokana na kazi anazozifanya Mfanyakazi huyo.
Aidha Bw. Mshomba alieleza kuwa, dhumuni kuu la kuanzishwa kwa Mfuko huo ni kutoa Mafao ya kutosha na stahili kwa Mfanyakazi aliyepatwa na maradhi au majeraha yaliyotokana na kazi anazozifanya Mfanyakazi huyo.
Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCD), Dkt. Abdulsalaam Omar, akimfafanulia mwananchi huyu aliyetembelea banda la Mfuko huo lililoko kwenye hema kubwa la Jakaya Kikwete, kwenye maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam 2017, barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam kuhusu hatua ambazo mfanyakazi anapaswa kuchukua baada ya kupata maradhi au kuumia wakati akitekeleza majukumu yake ya kikazi kabla ya kupatiwa Fidia na WCF.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), Bw. Masha Mshomba, akizungumza wakati akiwa kwenye banda la Mfuko huo. |
Mkuu
wa Kitengo cha Mawasiliano na
Uhusiano wa Mfuko huo, Bi. Laura Kunenge, (kulia), akizungumza na Posta
Masta Mkuu na Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania, Bw. Deo
Kwiyukwa, wakati alipotembelea banda hilo.
Mkurugenzi wa Huduma za
Tiba na Tathmini wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCD), Dkt. Abdulsalaam Omar,
akimfafanulia mwananchi huyu aliyetembelea banda la Mfuko huo lililoko
kwenye hema kubwa la Jakaya Kikwete, kwenye maonesho ya 41 ya biashara
ya kimataifa ya Dar es Salaam 2017, barabara ya Kilwa jijini Dar es
Salaam kuhusu hatua ambazo mfanyakazi anapaswa kuchukua baada ya kupata
maradhi au kuumia wakati akitekeleza majukumu yake ya kikazi kabla ya
kupatiwa Fidia na WCF.
Wafanyakazi
hawa wakipatiwa maelezo mbalimbali yahusuyo huduma zitolewazo na Mfuko
wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), walipotembelea banda la Mfuko huo
kwenye maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...