Mwanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, akipitia taarifa ya michango yake, baada ya kukabidhiwa na Maafisa wa Mfuko huo, alipotembelea banda la PSPF kwenye maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam, leo Julai 12, 2017. Wakati wa maonesho hayo yakitarajiwa kufikia kilele kesho Alhamisi Julai 13, 2017, zaidi ya watu 500 wametembeela banda la Mfuko huo hadi mchana huu na kati ya hao asilimia 70 walifika kujiunga na Mpango wa uchangiaji wa Hiari, (PSS), unaomuwezesha mwananchi yeyote ambaye anafanya kazi za kumuingizia kipato kuwa mwanachama. Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko huo, Bw. Abdul Njaidi, alisema na kuongeza faida za mwanachama kujiunga na PSS, ni pamoja na kupata bima ya afya. (NA K-VIS BLOG/Khalfan Said)
Afisa Msaidizi wa Uendeshaji wa PSPF, Bw.Mussa Mfaki, (kulia), akimkabidhi kadi ya kujiunga na PSPF kupitia Mpango wa uchangiaji wa Hiari, PSS, Bi.Damare B. Nampwani, leo Julai 12, 2017.
Mwananchi akijaza fomu ya lujiunga na PSPF kupitia Mpango wa PSS, huku Mwanasheria kutoka Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti MHifadhi ya Jamii, (SSRA), Bi.Imani Masebu, (kulia), na Mhandisi Ally Shanjirwa, (katikati), wakishuhudia.
Afisa Uhusiano wa PSPF, Bi. Coleta Mnyamani, (kulia), akimkabidhi kadi ya uanachama ya PSPF, Afisa wa Polisi wa Usalama Barabarani, Salvatory A. Chacky.
Hiki ndio kikosi kazi cha PSPF ambacho kwa takriban wiki moja na nusu kimekuwa kikitoa huduma kamambe kwenye banda la Mfuko huo kwenye jengo la Wizara ya Fedha na Mipango kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere, ambako kumekuwa na maonesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam. Kutoka kushoto waliosimama ni Isack Kimaro, Mussa Mfaki, Chaula Miteko, Mhandisi Ally Shanjirwa, Abdul Njaidi, Noah Amri,Win-God, Bw.Msina. Waliokaa kutoka kushoto, ni Bi. Coleta Mnyamani, Bi. Mariam Saleh, Bi. Irine Musetti na Bi. Asmahan H.Haji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...