Meneja wa mpango wa uchangiaji wa Hiari, (PSS), wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bi. Mwanjaa Sembe, (kulia), akimkabidhi kadi ya uanachama wa Mfuko huo kupitia mpango wa uchangiaji wa hiari, Mwanafunzi wa chuo cha Uhasibu (TIA), Bi.Demetriz Bayona, baada ya kujiunga na Mfuko huo leo Julai 2, 2017. 

Wananchi wengi waliotembelea banda la Mfuko huo leo, wamejiunga na mpango huo baada ya kupatiwa elimu na faida ambazo mwanachama anapata endapo atajiunga na mpango wa uchangiaji wa hiari ambapo kujiunga hakuna masharti isipokuwa kwa mtu yeyote mwenye kazi ya kumuingizia kipato na atatakiwa kuchangia au kuweka akiba ya kima cha chini cha shilingi elfu 10 kila mwezi. 

Miongoni mwa faifa ambazo mwanachama aliyejiunga na mpango huo ni pamoja na kujipatia bima ya afya, itakayomuwezesha kupata matibabu yeye mwanachama na wategemezi wake watatu. Lakini pia kujipatia mafao mablimbali yakiwemo fao la elimu, lakini pia mkopo wa nyumba na viwanja kutegemea na akiba ambayo mwanachama amejiwekea.
 Afisa kutoka Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Hifadhi ya Jamii, (SSRA), (kulia), akifuatilia jinsi maafisa wa PSPF wanavyotoa huduma kwa wanachama na wananchi wanaotembela banda la Mfuko huo. SSRA imeweka maafisa wake kila banda la linalotoa huduma ya hifadhi ya Jamii ili kusikiliza malalamiko ya wanachama husika wa Mfuko hiyo.
 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bw. William Erio, (kushoto), akikaribishwa na Afisa Uhusiano wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Bi. Coletha Mnyamani alipotembelea banda hilo leo Julai 2, 2017.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...