MJASIRIAMALI mdogo mkazi wa Chanika, jijini Dar es Salaam, Enos Marianus, amesema bahati nasibu ya Biko inayaoendelea kuchanja mbuga nchini Tanzania, utakuza uchumi wa washiriki na Watanzania kwa ujumla, akiwamo yeye ambapo ana mpango wa kuendeleza biashara zake..

Hayo yamesemwa na mshindi wa Sh Milioni 20 wa Biko, Marianus wakaati anakabidhiwa fedha zake katika makabidhiano yaaliyofanyika jana katika benki ya NMB, Posta, jijini Dar es Salaam.

Marianus alisema ukosefu wa ajira unasababisha watu wengi watamani kuingia kwenye ujasiriamali, hivyo uwapo wa mchezo wa Biko utapunguza changamoto hiyo, hivyo ni jambo la msingi la kuhakikisha kuwa kila mtu anacheza Biko ili ashinde mamilioni ya Biko.

“Nashukuru leo kwa kukabidhiwa fedha zangu Sh Milioni 20 kutoka kwa watu wa Biko, hivyo ninaamini kabisa mchezo huu utakuza uchumi wetu hususan sisi wajasiriamali wadogo ambao fedha hizi zitaingia kwenye kupanua wigo wa biashara zetu kwa namna moja ama nyingine,” Alisema.

Naye Mratibu wa Matukio na Mawasiliano wa Biko, Hassan Melles, alisema ushindi wa Biko ni rahisi husuan kwa wale wanaocheza mara nyingi kwa kufanyaa miamala kwenye simu za Tigo Pesa, M-Pesa na Airtel kuanzia Sh 1,000 na kuendelea ambapo namba yao ya kampuni ni 505050 na ile ya kumbukumbu ni 2456.

“Sh 1,000 ya Biko inayochezwa inampa mtu ushindi wa papo kwa hapo kuanzia Sh 5,000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni Moja inayolipwa papo hapo kwenye simu iliyotumika kuchezea Biko pamoja na zawadi nono ya Sh Milioni 20 inayotoka Jumatano na Jumapili,” Alisema Melles.

Zaidi ya Sh Bilioni moja tayari zimelipwa kwa washindi wa Biko kwa kipindi cha mwezi Mei na Juni pekee, ikiwa ni mwendelezo wa kutoa mamilioni ya fedha kwa washindi wake wanaocheza Biko tangu kuanzishwa kwa mchezo huo hapa nchini.
 Meneja Masoko wa Biko Tanzania, Goodhope Heave wa pili kutoka kulia akimkabidhi fedha zake mshindi wa Sh Milioni 20 wa Biko, Enos Marianus mwenye shati jeupe, jana jijini Dar es Salaam, katika benki ya NMB. Wa kwanza kulia ni Mratibu wa Matukio na Mawasiliano wa Biko Tanzania, Hassan Melles.
 Mratibu wa Matukio na Mawasiliano wa Biko Tanzania, Hassan Melles wa pili kutoka kulia akimkabidhi fedha zake mshindi wa Sh Milioni 20 wa Biko, Enos Marianus mwenye shati jeupe, jana jijini Dar es Salaam, katika benki ya NMB. Wa kwanza kulia ni Goodhope Heaven, Meneja Masoko wa Biko Tanzania.
Mshindi wa Sh Milioni 20 wa Biko droo ya 24, Enos Marianus kulia aakiwa na furaha tele baada ya kukabidhiwa fedha zake jana katika benki ya NMB, jijini Dar es Salaam, siku moja baada yaa kutangazwa mshindi wa bahati nasibu ya Biko. Kushoto kwake ni mkewe Bi Kisa Kasito aliyemsindikiza katika kukabidhiwa fedha zake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...