Na
Felix Mwagara (MOHA)
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi
Hamad Masauni amelitaka Jeshi la Polisi mkoani Manyara kufungua Kituo cha
Polisi katika Makazi ya Kabila la Wahazabe wanaoishi katika Bonde la Yueda
Chini, wilayani Mbulu.
Masauni alisema hayo jana wakati
akizungumza na mamia ya wananchi wa kabila
hilo mara baada ya kukagua jengo la mifugo katika eneo la bonde hilo
ambalo jamii hiyo ilijitenga kwa kuweka makazi pembezoni mwa Mji wa Mbulu.
“Hivi karibuni Kituo cha Polisi
kitafunguliwa hapa ili kulinda usalama wenu katika eneo hili ambalo lilikua
halina kituo cha Polisi kwa miaka mingi. Serikali ya Rais Magufuli ni sikivu
ndio mana nimekuja hapa kuwasikiliza matatizo yenu na kuwatekelezea.” Alisema
Masauni huku akishangiliwa na wananchi hao.
Aliongeza kuwa, mchakato wa kujenga
kituo hicho umeanza na tayari ametoa maelekezo kwa Kamanda wa Jeshi la Polisi
wa Mkoa huo, kwa kushirikiana na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu,
Wabunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini na Mbulu Mjini.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi
Hamad Masauni (watatu kushoto) na Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini, Flatei
Massay (wapili kulia) wakicheza ngoma ya Wabarbaig/Watatoga kabla ya Masauni
kuzungumza na mamia ya wananchi wa Kabila maarufu la Wahazabe na makabila
mengine yaliyopo katika Bonde la Yueda Chini, Wilaya ya Mbulu mkoani Manyara.
Masauni aliiagiza Jeshi la Polisi mkoani humo, kujenga Kituo cha Polisi kwa
uharaka ili jamii hiyo ambayo inaishi pembezoni mwa mji wa Mbulu.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi
Hamad Masauni akizungumza na mamia ya wananchi wa Kabila maarufu la Wahazabe na
makabila mengine yaliyopo katika Bonde la Yueda Chini, Wilaya ya Mbulu mkoani
Manyara. Masauni aliiagiza Jeshi la Polisi mkoani humo, kujenga Kituo cha
Polisi kwa uharaka ili jamii hiyo iweze kupata ulinzi wa kutosha katika eneo
hilo.
Wananchi wakimshangilia Naibu Waziri wa Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (hayupo pichani) wakati alipowatangazia
kufunguliwa Kituo cha Polisi hivi karibuni katika Kijiji cha Bonde la Yueda
Chini, lililopo wilayani Mbulu, Mkoa wa Manyara.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi
Hamad Masauni akijadiliana na maafisa wa halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, mkoani
Manyara pamoja na watendaji mbalimbali wa wilaya hiyo, ndani ya jengo la mifugo
lililopo Yaeda Chini katika makazi ya Wahazabe, ambalo linatarajiwa kufunguliwa
Kituo cha Polisi. Kulia ni Mkuu wa Jeshi la Polisi mkoani Manyara (RPC), Francis
Massawe, na kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini, Flatei Massay.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi
Hamad Masauni (kushoto), akimsikiliza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Francis
Massawe alipokuwa akijibu maswali mbalimbali ya uhalifu ambayo yaliulizwa na
wananchi (hawapo pichani) wa Kijiji cha Yueda Chini Wilaya ya Mbulu mkoani
humo, ambalo kuna makazi ya jamii ya Kabila la Wahazabe. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...