Mtanzania Augustino  Mponzi anayeishi jijini Dallas, Texas, Marekani, amebuni mchezo marufu wa karata uitwao ALBASTINI kwa njia ya mtandao. Mchezo huu unaweza kuchezwa kwa kutumia simu ya mkononi pamoja, tablet pamoja na iPad, na iPad Touch.
Hivi sasa Tino Bw. Mponzi ameandaa mashindano ya ALBASTINI ambayo anasema watu wote duniani kuliko na internet wanaweza kucheza kwa kutumia simu za mkononi. Tayari ameshatengeneza Application zinazomwezesha mtu mwenye simu za Android  pamoja na tablet zenye kutumia Google play hali kadhalika wenye kutumia iPhone,  iPad na iPad Touch wanaweza kushiriki kwani App ya iOS inawezesha mchezo huo kupakuliwa na kuwekwa (install) kwenye vifaa hivyo.

“Kuingia kwenye mashindano ni bure na mshidndi atapata Apple iPad”, anasema Bw. Mponzi, akiongezea kwamba baada ya kupakua (install) application hiyo mdau utapata maelekezo yote ya namna ya kucheza. Link za mchezo huo ni hizi hapa chini. KAZI KWAKO mpenzi wa ALBASTINI>



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...