Muhitimu wa shahada ya computer science, Magdalena Uronu akionyesha bidhaa zake anazotengeneza yeye katika Maonyesho ya 41 ya biashara yanayoendelea jijini Dar es Salaam. Magdalena anayejulikana kama mkurugenzi wa Megy Precious watengenezaji wa bidhaa zenye asili na utamaduni wa kiafrika kama mikoba Viatu bangili na heleni amasema ameamua kujiajiri baada ya kuona kuna fursa ya kufanya hivyo na siyo kutegemea ajira tu. Amesema biashara hiyo aliyoianza muda mfupi baada ya kupata stashahada yake imemuwezesha kuajiri vijana watatu wa kumsaidia katika shughuli hio.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...