Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Rashid Ali Juma mwezi ujao,anatarajia kuzindua msafara wa magari ya zamani mjini humo ili kuamsha aina mpya ya utalii.

Msafara huo unatarajiwa kuanzia Hyatt Park hoteli iliyopo mjini Zanzibar na kumalizikia Melia hoteli Kiwengwa.

Waziri Juma amesema hayo leo na kuongeza kuwa lengo la safari hiyo ni kuamsha aina mpya ya utalii itakayopelekea watalii wengi kuja nchini.

Amesema magari hayo ya miaka ya 60 yalikuwa yakitumiwa na wafalme na masultani, lakini hadi leo yanaweza kutembea."Utalii unachangia pato la Zanzibar kwa asilimia 27 huku ukichangia asilimia 80 ya fedha za kigeni kwani mambo mengi ya kitalii yamekuwa ya kawaida".

Amesema kwa kushirikiana na Hyatt hoteli tumekuja na mbinu mpya ya kuwavutia watalii wengi zaidi.Amesisitiza kuwa hakutakuwa na mbio za magari bali ni msafara wa magari hayo ya zamani ambayo yatatembea umbali wa kilomita 30 na kwa kuanzia yatakuwa magari sita, matatu ya watu binafsi na matatu ya Hyatt.

Aidha amewahakikishia usalama wa kutosha katika msafara huo ambapo vyombo vya ulinzi vitakuwa vikisindikiza mwanzo mpaka mwisho wa safari.
Nae Meneja mkuu wa Hyatt hoteli Garry Friend alisema msafara huo utaanzia Hyatt park hoteli Zanzibar ukipitia mji mkongwe na kumalizikia Melia Kiwengwa Agosti 26 ambayo ndiyo siku ya ufunguzi rasmi. 

Amesema lengo la kutumia magari hayo yaliyotumika miaka ya 60 ni kusisimua utalii."Watu wengi watavutiwa na aina hii ya utalii" alisema Friend.
 Waziri wa Habari utalii Utamaduni Sanaa na Michezo Mh.Rashidi Juma Kushoto Akizungumza na Waandishi wa Habari mapema Jijini Leo
Kulia ni Meneja Mkuu wa Hyat Hotel Bwn Garry Friend

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...