MSTAAFU wa utumishi wa umma, Bi. Marcella Isidori Chanda, amewahimiza wananchi na wastaafu wenzake, kujiunga na Mfuko wa Pensehni wa PSPF, kupitia mpango wake wa uchangiaji wa Hiari, (PSS), kwani kuna faida nyingi mwanachama atazipata.

Bi. Chanda, ameyasema hayo muda mfupi baada ya kujiunga na Mpango huo wa PSS, leo Julai 10, 2017, baada ya kupatiwa elimu ya huduma zitolewazo na PSPF kwa wanachama wake.

“Mimi nilikuwa mtumishi wa benki na nimestafu mwaka 2013, ni meona iko haja ya kujiunga na mpango huu ambao hatimaye moja ya mambo yaliyonivutia ni kupatiwa bima ya afya, kwani nimeelzwakuwa ukiwa mwanachama wa PSS, basi unapata sifa za kujiunga na bima ya Afya, tofauti na ukiwa mtu binafsi gharama zinakuwa kubwa mno na zinafikia hadi shilingi 1,500,000nkwa mwaka.” Alisema Bi. Chanda.

Akieleza zaidi, Bi. Chanda alisema, amefikia uamuzi wa kujiunga naPSPF, baada ya kupata taarifa nyingi kupitia vyombo vya habari kuwa, lakini pia majirani na jamaa zngu kuwa wamekuwa wakifaidika na huduma ya afya kupitia bima ya afya.

Mstaafu huyo alsiema, leo amejiunga na PSS na pia atamueleza mumewe naye pia ajiunge. “Natoa wito wka wastaafu wenzangu na wananchi kwa ujumla kujiunga na PSPF ili kujihami na gharama za matibabu. Kwa upande wake, Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Bw. Abdul Njaidi alisema, karibu asilimia 60 ya wananchi wanaofika kwenye banda hilo, wamekuwa wakijunga na Mpango wa PSS na moja ya sababu kubwa ni kupatiwa bima ya Afya.


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani, (kulia), akizungumza jambo mbele ya Afsia Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Bw. Abdul Njaidi alipotembelea banda la Mfuko huo leo Julai 10, 2017.
Mkurugenzi wa Mawasiliano na Elimu kwa Umma, wa Mamlaka ya Udhibiti na Usimamizi Hifadhi ya Jamii, (SSRA), Bi. Sarah Kibonde Msika, (kushoto) akimsikiliza Bw. Njaidi kwenye banda la PSPF, Julai 10, 2017. SSRA imeweka maafisa wake katika kila banda la Mifuko ya Hifadhio ya Jamii, ili kufuatilia utoaji huduma wa Mifuko hiyo kwa wananchi kwenye maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam.


Afasia Msaidizi wa Uenddshaji wa PSPF, Bw. Win-God Simon, (kushoto), akiwahudumia maafisa hawa wa polisi ambao ni wanachama wa Mfuko.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...