Moja kati ya huduma zitolewazo na  Sukos Foundation mbali na Disaster Management pia ni kusaidia familia zisizojiweza. Kwa kulitambua hilo, Bernedicta John akiwa Ni mmoja wa watoto walio na ugonjwa wa saratani ya ngozi ( Skin Cancer) ambae pia anatoka katika Familia ya hali ya chini ( Destitute family) Sukos inashirikiana kumsaidia kijana  huyo pamoja na wengine kama hawa wanaotoka katika familia duni na pia kupata nafasi za kutimiza malengo yao.
Siku ya Leo, baada ya kujua kuwa moja ya ndoto kubwa za Mtoto huyu ni kuwa mchezaji mpira mahiri nchini Tanzania na duniani, na mchezaji anayempenda sana, ama  " Role Model" wake ni mchezaji wa Taifa Stars Na Simba Sports Club Ramadhan Shiza Kichuya. Sukos imefanikiwa  kumkutanisha mtoto huyu namoja na Role model wake Mchezaji Shiza Kichuya ambae amemkabidhi Jezi yenye Jina lake pamoja na kumpa misaada mengine mbalimbali kumsaidia Mtoto huyu anaetoka katika familia duni kutimiza ndoto yake. Hakika Ilikua ni siku ya furaha kubwa sio kwa Sukos pekee bali pia kwa Bernedicta na mwanasoka Ramadhan Shiza Kichuya pia!

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...