Naibu Spika Dr. Tulia Ackson kupitia Taasisi yake ya Tulia Trust ameanza ziara ya siku 10 mkoani Mbeya kazi kubwa ikiwa ni kutoa misaada kwa Taasisi mbalimbali zikiwemo shule na hospitali huku akikagua maendeleo ya baadhi ya Taasisi alizozisaidia katika siku za nyuma.

Dr. Tulia katika ziara yake ya jana alikabidhi misaada vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya Tsh. 1.1m kwa Shule ya Msingi Lubwe, Tsh. 2.5m kwa Shule ya Sekondari Nkunga, vitanda 20 kwa Hospitali ya Igongwe pamoja na kukagua ujenzi wa Vyoo na Bafu kwa wajawazito katika Hospitali ya Makandana.
Naibu Spika Dr. Tulia Akson akiwa amembeba mmoja wa watoto yatima katika Hospitali ya Igogwe
Naibu Spika Dr. Tulia Akson akivuka Daraja la Nkunga-Lupepo lililopo Rungwe
Naibu Spika Dr. Tulia Akson akisoma moja ya bango lililowekwa na wananchi wakati wa ziara yake

Naibu Spika Dr. Tulia Akson akiwa kwenye picha picha ya pamoja na Wanafunzi wa Shule ya Msingi Rungwe
Naibu Spika Dr. Tulia Akson akisalimiana na wazazi katika Hospitali ya Igogwe ambayo haina eneo la kupumzikia wakinamama baada ya kujifungua

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...