Shirika la ndege la Kitanzania Precision Air limezindua kwa
mafanikio safari zake za kwenda Entebbe. Ndege ya uzinduzi wa safari hizo iliondoka Jijini Dar es Salaam majira ya saa 1:10 asubuhi leo kuelekea Entebbe na kuwasili Entebbe majira ya saa 4:50 Asubuhi na kupokewa kwa salamu
maalumu ya kumwagiwa maji na magari ya zima moto, ikiwa ni ishara ya kuanza rasmi kwa
zama mpya za huduma za Precision Air kati ya Tanzania na Uganda.
Akizungumzia kuanza rasmi kwa safari hizo Meneja Uratibu na Mahusiano Bw. Hillary Mremi
amesema kuwa, kupitia safari za Precision Air Tanzania na Uganda wamehakikishiwa usafiri wa
uhakika.
“Tutakuwa tukifanya safari mara tatu kwa wiki, kila siku ya Jumatatu, Alhamisi na Jumamosi na
baadaye kuongeza safari kulingana mahitaji ya soko.” Amekaririwa Bw. Mremi
Precision Air iliahirisha safari za Entebbe mnamo mwaka 2013 kupisha maboresho ya mtandao
wa wa safari zake katika kuhakikisha inazingatia tija katika shughuli zake.
Precision Air ndilo Shirika pekee la ndege linalotambuliwa na IATA ambalo linafanya safari za
moja kwa moja kati ya Tanzania na Uganda. Inatarajiwa safari hizi za Precision zitaimarisha
mahusuano ya kiuchumi na kidiplomasia kati ya Tanzania na Uganda, hasa ikizingatiwa kuwepo
kwa miradi mbali mbali ya pamoja kama ule wa bomba la mafuta litakalo anzia nchini Uganda
hadi Tanzania.Ni miradi kama hiyo inayotarijiwa kunufaika na safari za Precision Air kwa
kufanikisha miradi hiyo kwa wakati.
Precision Air ilianzishwa mnamo mwaka 1993 kama shirika binafsi la ndege za kukodi,Shirika la
ndege la Precision Air limeendelea kukua na kuwa moja ya mashirika ya ndege ya
nayoheshimika Africa Mashariki na Africa kwa ujumla.Kwa sasa Shirika hilo linafanya safari za
ndani na nje kuelekea sehemu takribani 11. Iktokea Dar es Salaam (makao makuu) Precision Air
inasafiri kuelekea Arusha, Bukoba, Kigoma, Kilimanjaro, Musoma, Mtwara, Mwanza, Tabora,
Zanzibar na Nairobi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...