Kwa mwaliko maalum Waziri mstaafu wa Tanzania Profes Mark Mwandosya anahudhuria Mkutano Mkuu wa 19 wa Umoja wa Mashirika ya Umeme ya Afrika unaofanyika Livingstone, Zambia. Mkutano Mkuu huo umefunguliwa jumatano tarehe 12 Julai 2017 na Mhe. Edgar Chagwa Lungu,Rais wa Jamhuri ya Zambia.
Katika hotuba yake Rais Lungu amesisitiza umuhimu wa umeme katika maendeleo ya Zambia na aliwaambia Wajumbe kuwa hakuwa tayari kuona Shirika la Umeme la Zambia(ZESCO) likishindwa kutoa huduma stahiki na kushindwa kutekeleza miradi ya maendeleo kutokana na hali mbaya ya kifedha.
Hivyo basi hivi karibuni ameruhusu ZESCO kuongeza bei ya umeme kwa asilimia 75. Amesema kitendo hicho ni sawa na kujiua kisiasa lakini yuko tayari kuikosa Ikulu mwaka 2021 kuliko kuiona umeme unakosekana, uchumi unazorota na ZESCO inakufa.
Rais wa Zambia Mhe. Edgar Lungu akitoa hotuba ya kufungua Mkutano huo
Profesa Mark Mwandosya akitoa mada kuhusu Changamoto za Udhibiti (Regulation) katika Sekta ya Umeme Afrika.
Profesa Mark Mwandosya akiwa na Mama Lucy Mwandosya wakimsikiliza Mhe. Rais Lungu. |
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...