Kwa mwaliko maalum Waziri mstaafu wa Tanzania  Profes Mark Mwandosya anahudhuria Mkutano Mkuu wa 19 wa Umoja wa Mashirika ya Umeme ya Afrika unaofanyika Livingstone, Zambia. Mkutano Mkuu huo umefunguliwa jumatano tarehe 12 Julai 2017 na Mhe. Edgar Chagwa Lungu,Rais wa Jamhuri ya Zambia.
Katika hotuba yake Rais Lungu amesisitiza umuhimu wa umeme katika maendeleo ya Zambia na aliwaambia Wajumbe kuwa hakuwa tayari kuona Shirika la Umeme la Zambia(ZESCO) likishindwa kutoa huduma stahiki na kushindwa kutekeleza miradi ya maendeleo kutokana na hali mbaya ya kifedha. 
Hivyo basi hivi karibuni ameruhusu ZESCO kuongeza bei ya umeme kwa asilimia 75. Amesema  kitendo hicho ni sawa na kujiua kisiasa lakini yuko tayari kuikosa Ikulu mwaka 2021 kuliko kuiona umeme unakosekana, uchumi unazorota na ZESCO inakufa. 

 Rais wa Zambia Mhe. Edgar Lungu akitoa hotuba ya kufungua Mkutano huo
 Profesa Mark Mwandosya  akitoa mada kuhusu Changamoto za Udhibiti (Regulation) katika Sekta ya Umeme Afrika. 
Profesa Mark Mwandosya akiwa na  Mama Lucy Mwandosya wakimsikiliza Mhe. Rais Lungu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...