Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Mhe. Benjamini William Mkapa akikata utepe kuashiria ufunguzi wa jengo jipya la upasuaji kwenye kituo cha afya cha Nkomo kilichopo kijiji cha Mwalushu,Wilayani Itilima-Simiyu
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Itilima Dkt. Anold Musiba akitoa maelezo kwa Rais Mstaafu,kulia ni Balaozi wa Japan nchini Tanzania Mhe.Masaharu Yoshida. Jengo hilo limejengwa na Ubalozi wa Japan kupitia Taasisi ya Benjamini Mkapa na kugharimu kiasi cha shilingi za kitanzania milioni 270.
Rais Mstaafu akiangalia moja ya vifaa vilivyomo kwenye chumba cha upasuaji .Ujenzi wa jengo hilo kwa asilimia kubwa itawasaidia akina mama wajawazito ambapo awali wananchi wa kijiji hicho walikua wakitembea kilometa arobaini kwenda kupata huduma za namna hiyo.
Jengo hilo la upasuaji linavyoonekana
Msimamizi wa ujenzi wa jengo hilo kutoka Taasisi ya Benjamini Mkapa Geofrey Nyaluke (mwenye fulana ya jano) akitoa maelezo kwa Viongozi waliofika kushuhudia ufunguzi wa jengo hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...