Mkurugenzi wa Global Education Link (GEL), Abdulmalik Mollel amesema kuwa katika serikali ya viwanda wakuu wa shule wanaweza kujenga msingi mzuri kwa wanafunzi kwani ni rasilimali katika sekta hiyo.

Mollel aliyasema hayo wakati wa Rais wa Umoja wa Shule za Sekondari nchini (Tahossa)alipotembelea banda la Global Education Link katika maonesho ya 41 ya biashara ya Kimataifa katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam, Mollel amesema kuwa wa wakuu wa shule ndio wanaweza kuchukua dhamana ya serikali ya kauli ya Rais Dk. John Pombe Magufuli kuwa serikali ya awamu katika dhana ya viwanda.

Mollel amesema kuwa serikali ya viwanda inahitaji watu wa masomo wa sayansi, sanaa na masoko kwa pamoja ndio wanajenga viwanda.

Aidha amesema kuwa Global itaendelea kushirikiana wakuu wa sekondari katika ujenzi wa nchi ya viwanda.

Naye Rais wa Umoja wa Wakuu wa Sekondari Nchini (Tahossa) Mwalimu Vitaris Shija amesema kuwa Global Education Link (GEL) ni chombo ambacho kinafanya wanafunzi wapende masomo ya sayansi ambao ndio watakaotumika katika sekta ya viwanda.

Amesema kuwa sekta ya viwanda inahitaji wataalam wa sayansi, sanaa na biashara ndio mahitaji ya sekta ya viwanda kwa sasa kutokana na kauli ya Rais Dk. John Pombe Magufuli kuwa serikali ya awamu ya tano ni serikali ya viwanda.

Shija amesema kuwa Global Education Link imeleta chachu ambapo inatakiwa kuanza kushawishi wanafunzi kusoma sayansi kuanzia shule ya msingi kutokana na mahitaji ya sekta ya viwanda.

Shija amesema kuwa kutokana na mahitaji ya rasilimali katika sekta ya viwanda wakiwa wakuu wa shule za sekondari kuzungumza suala hilo kuanzia kwa wazazi juu ya nchi mahitaji yar rasimali katika sekta yaya viwanda.

Amesema kuwa serikali kulipa wataalam wa nje ni gharama ambao sehemu kubwa watalipwa na kwenda kujenga kwao lakini wanafunzi wa waliokwenda watafanya kazi nchini na kujenga nchi yao.
 Mkurugenzi wa Global Education Link , Abdulmalik Mollel akiwa na Rais wa Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari Nchini (Tahosa) Mwalimu Vitaris Shija katika Maonesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa katika viwanja vya Mwalim Nyerere jijini Dar es Salaam.
 .Mkuu Idara ya Masoko kwa Njia ya Mtandao, Micky Musa akionesha mfumo wa Taarifa za wanafunzi wanaosoma nje kupitia Global Education Link (GEL) katika Maonesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa katika viwanja vya Mwalim Nyerere jijini Dar es Salaam.


Picha mbalimbali za mafisa za Global Education Link (GEL) katika katika Maonesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa katika viwanja vya Mwalim Nyerere jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...