RAIS
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein,
amerejea nchini leo akitokea nchini Uingereza.
Katika
uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, viongozi mbali mbali wa
vyama vya siasa na Serikali pamoja na wakuu wa vikosi vya ulinzi na usalama wa
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
walimpokea Dk. Shein wakiongozwa na Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi
Seif Ali Idd.
Dk.
Shein katika safari hiyo maalum ya nchini Uingereza, alifuatana na Mkewe Mama
Mwanamwema Shein pamoja na Watendaji wengine wa Serikali.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk, Ali Mohammed Shein akiteremka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Zanzibar akitokea Uingereza kwa ziara maalumu
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk, Ali Mohammed Shein akisalimiana na Makamo wa Pili wa Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar Balozi Seif Ali Idi mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Zanzibar akitokea Uingereza kwa ziara maalumu
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk, Ali Mohammed Shein akisalimiana na Viongozi mbalimbali waliofika kumpokea baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Zanzibar akitokea Uingereza kwa ziara maalumu
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk, Ali Mohammed Shein akisalimiana na Viongozi mbalimbali waliofika kumpokea baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Zanzibar akitokea Uingereza kwa ziara maalumu.
Picha na IKULU na Yussuf Simai - MAELEZO ZANZIBAR.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...