Ndugu, Jamaa, Marafiki, wanafamilia na wote  tuliopatwa na msiba huu wa marehemu Professor  Henslay William Kabisama uliyotokea huko Ontario, California, Marekani, mnaarifiwa kwamba familia itawasili siku ya Jumatano Julai 19, 2017 usiku na maombolezo yataanza siku hiyo hiyo  nyumbani kwa marehemu Ursino  Victoria nyuma ya Ofisi za Halotel.

Siku ya Ijumaa  Julai 21, 2017 Mwili wa mpendwa wetu Prof Henslay Kabisama utawasili  uwanja wa ndege wa Julius Nyerere saa tisa mchana.
Mazishi yanatarajiwa kufanyika siku ya Jumamosi Julai 22, 2017  katika makaburi ya Kinondoni, yakitanguliwa na ibada ambayo itafanyika  katika kanisa la   St Alban Upanga saa saba kamili mchana.
 Bwana alitoa na bwana ametwaa jina bwana libarikiwe - AMEN.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...