Ndugu, Jamaa, Marafiki, wanafamilia na wote tuliopatwa na msiba huu wa marehemu Professor Henslay William Kabisama uliyotokea huko Ontario, California, Marekani, mnaarifiwa kwamba familia itawasili siku ya Jumatano Julai 19, 2017 usiku na maombolezo yataanza siku hiyo hiyo nyumbani kwa marehemu Ursino Victoria nyuma ya Ofisi za Halotel.
Siku ya Ijumaa Julai 21, 2017 Mwili wa mpendwa wetu Prof Henslay Kabisama utawasili uwanja wa ndege wa Julius Nyerere saa tisa mchana.
Mazishi yanatarajiwa kufanyika siku ya Jumamosi Julai 22, 2017 katika makaburi ya Kinondoni, yakitanguliwa na ibada ambayo itafanyika katika kanisa la St Alban Upanga saa saba kamili mchana.
Bwana alitoa na bwana ametwaa jina bwana libarikiwe - AMEN.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...