Mkuu
wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Paul Makonda leo ametoa siku saba
kwa Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam DCP Lucas
Mkondya kuhakikisha wizi wa vifaa vya Magari unakomeshwa mara moja.
Akitoa
maagizo hayo, Mheshimiwa Makonda amesema wizi wa vifaa vya magari
vikiwemo Vioo, Radio, Side mirrow, Power Window,Taa pamoja na Shoo ya
mbele na nyuma ya Gari vimekuwa vikishamiri kila kukicha jambo
linalowakera wananchi na kuwapa hofu ya kuweka magari yao kwenye
maegesho kwa kuhofia kuibiwa kitendo ambacho amesema hakivumiliki.
“Sitaki
kusikia watu wanaibiwa vifaa vya Magari yao,watu wanaibiwa Vioo, Power
Window,Radio, Taa,Side Mirror na wakati mwingine wanavunja vioo vya gari
na kuiba Pochi na Laptop, sasa haiwezekani wizi wa namna hii uendelee
kwenye Mkoa wangu, sasa Kaimu Kamanda Kanda Maalumu nakuagiza na
ninakupa siku saba sitaki kusikia wizi wa vifaa vya magari ukiendelea,
nataka ifikie hatua mtu aweze kuegesha Gari lake na kulikuta likiwa
salama” Alisema Makonda.
“Mwananchi yoyote
atakaeibiwa na akapeleka taarifa Polisi na hatua za kisheria zichukuliwe
atoe taarifa kwangu bahati nzuri wananchi wana namba zangu, haiwezekani
Mwananchi anajikusanya na kununua gari alafu anaibiwa watu wanaiba
vifaa vyake, wizi wa namna hii nasema Mwisho ndio umefika leo,"
Alisisitiza Makonda.
Aidha Makonda ameagiza
Maduka na Vijiwe vyote vinavyouza vifaa vya Magari kujisajili mara moja
iliviweze kutambulika na Serikali.“Kinachoshangaza
ni kwamba hawa wanaoiba wana vijiwe vyao ambapo wanauza hivyo vifaa,
ukienda Kariakoo, Magomeni na pia Temeke (Keko) kuna vijiwe ambavyo
ukienda kule unakuta kifaa kilichoibiwa kwenye Gari lako kipo mtaani
kinauzwa” Aliongeza Makonda.
Akipokea Maagizo
hayo, Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam DCP Lucas
Mkondya amesema kuwa maagizo hayo yanaanza kutekelezwa leo ambapo msako
utaanza leo kuhakikisha Genge la wezi wa vifaa vya magari
vinasambaratishwa.
Aidha amewaagiza Makamanda
wa polisi Temeke, Ilala na Kinondoni kuanza utekelezaji wa maagizo hayo
kuanzia leo na kuwataka wote wanaouza vifaa vya wizi kujisalimisha mara
moja kwa Jeshi la Polisi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...