Ijumaa Julai 15,2017,Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack ametembelea kiwanda cha kutengeneza mafuta ya mchele kinachomilikiwa na kampuni ya Mwekezaji kutoka nchi ya China Jielong Holding kilichopo katika kijiji cha Nhelegani kata ya Kizumbi katika manispaa ya Shinyanga.

Mkuu huyo wa mkoa aliyekuwa ameambatana na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Shinyanga na maafisa mbalimbali mkoa huo amejionea jinsi kampuni hiyo ilivyodhamiria kuzalisha mafuta ya kupikia yanatokana na mapumba laini ya mpunga “Mchele”. 

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Telack alisema kiwanda hicho ni cha pekee nchini Tanzania na Afrika kwa ujumla na kitasaidia wamiliki wa mashine za kukobolea mpunga pamoja na wakulima kunufaika na zao la mpunga kwani wataweza kuuza mapumba kwa ajili ya kutumika kama malighafi kuzalishia mafuta hayo. 

“Niwapongeze wawekezaji hawa kwa ubunifu huu wa kiwanda cha aina yake, serikali ya mkoa wa Shinyanga inaunga mkono jitihada za kuhakikisha tunakuwa na uchumi wa viwanda,tushirikiana kuwahamasisha wananchi kulima mpunga kwa wingi na wale wenye mpunga basi wauze mapumba yao ili wajipatie kipato”,alieleza Telack. 

“Naamini watu wenye mashine za kukobolea mpunga wataongeza kipato kwa kuuza mabaki ya mpunga kwa ajili ya kuendeshea kiwanda hiki ambacho pia kinazalisha nishati ya umeme kwa kutumia mapumba”,alieleza Telack. 
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack (kulia) akitembelea kiwanda cha kutengeneza mafuta ya mchele kinachomilikiwa na kampuni ya Mwekezaji kutoka nchi ya China Jielong Holding kilichopo katika kijiji cha Nhelegani kata ya Kizumbi katika manispaa ya Shinyanga.Kulia kwake ni Mkalimani katika kampuni hiyo Joseph Warioba akifuatiwa na Mwenyekiti wa kampuni Jielong Holding,Qi Qi Shuwei.Wengine ni wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Shinyanga na maafisa kutoka mkoa huo. 
Qi Shuwei akiongoza msafara wa mkuu wa mkoa wa Shinyanga kuangalia uzalishaji wa bidhaa mbalimbali zinazotokana na mazao yanayolimwa na wakulima. 
Mkalimani katika kiwanda cha Jielong Holding,Joseph Warioba akitoa maelezo kwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Zainab Telack kuhusu malighafi mbalimbali zinazotumika katika kiwanda hicho cha kutengeneza mafuta ya alizeti,pamba,mchele na sabuni. 
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akingalia shughuli ya uzalishaji mafuta ya alizeti inavyofanyika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...