Na Benny Mwaipaja, WFM-Dodoma

Serikali imeeleza kuwa inajitahidi kuboresha miundombinu kama vile teknolojia ya Mawasiliano, Barabara, Ulinzi, Maji na Umeme katika maeneo ya vijijini ili kuweka mazingira bora yatakayovutia wawekezaji kutoka sekta binafsi kuwekeza katika sekta ya fedha ili kupanua huduma hiyo katika maeneo ya mijini na vijijini.

Hayo yameelezwa Bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Josephine Chagulla (CCM), aliyetaka kujua mpango wa Serikali wa kuwapa wanawake elimu kuhusu mikopo pamoja na kufikisha huduma za kibenki maeneo ya vijijini ili waweze kufikiwa na huduma za kifedha.

Mhe. Josephine Chagulla ameeleza kuwa wanawake wengi wa vijijini hawakopesheki kwa sababu benki haziwafikii, pia hawana mafunzo maalumu ya kuwasaidia ujuzi wa namna ya kuzifikia huduma hiyo ya kukopeshwa

Akijibu swali hilo Dkt. Kijaji alisema kuwa, elimu ya fedha inahusisha wadau mbalimbali ikiwemo Serikali na Taasisi zake, ambapo kwa upande wa Serikali, Benki Kuu inaratibu uanzishwaji wa taasisi ya kitaifa itakayokuwa na jukumu la kuratibu, kuwezesha na kusimamia utoaji wa elimu ya fedha kwa jamii.

“Serikali kupitia Benki Kuu imetoa mwongozo wa Uwakala wa Huduma za Kibenki ili kupanua wigo wa huduma za kibenki kuweza kuwafikia wananchi wengi zaidi na kwa gharama nafuu hasa katika maeneo ya vijijini”. Alisema Dkt. Kijaji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...