Na Haji Nassor (OUT), Pemba
Kiasi cha shilingi bilioni 39.7 kati ya shilingi bilioni 42 zilizotolewa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya juu Zanzibar ‘BMEJZ’ kwa ajili ya kuwakopesha wanafunzi waliosoma elimu ya juu, ziko mikononi mwa wadaiwa hao, kuanzia mwaka 2006 hadi mwezi Juni mwaka huu.
Wakati fedha hizo zikiwa mikononi mwa wadaiwa, tayari shilingi bilioni 2.3 ndizo pekee, zilizokwisharejeshwa na wakopaji, ambapo kati ya hizo shilingi bilioni 42, shilingi bilioni 7.7 Bodi hiyo ilizirithi kutoka kwa uliokuwa mfuko wa elimu ya juu Zanzibar, ambao ulikoma kufanya kazi zake mwaka 2011.
Bodi hiyo ya mikopo ya elimu ya juu, kila mwezi hukusanya wastani wa shilingi milioni 100, kutoka kwa wakopaji ambao ni wanafunzi kila mwezi hadi mwezi Juni mwaka huu wa 2017.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...