Na Lulu Mussa, Dodoma.

Serikali ya Tanzania kupitia Mfuko wa Mabadiliko ya Tabianchi (Green Climate Fund) imepata fedha za kutekeleza mradi mkubwa wa maji kutoka Ziwa Victoria hadi Mkoa wa Simiyu ambapo fedha za Mradi huo zitapitia Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW).

Hayo yamesemwa leo na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Prof. Faustin Kamuzora wakati wa kikao kazi kilichojumuisha wadau wanaohusika na utekelezaji wa Mradi wa maji wa Simiyu, mradi unaofadhiliwa na Mfuko wa mabadiliko ya tabianchi ambapo imebainika kuwa utekelezaji wake utaanza mara moja.

Aidha, Prof. Kamuzora amesema kuwa fedha hizo zinapitia Benki ya Maendeleo ya Ujerumani kutokana na sababu kwamba Serikali ya Ujerumani imekua ikifadhili miradi mbalimbali ya maji hapa nchini. “Ili kupata fedha kutoka katika mfuko huu ni lazima zipite kwenye taasisi ambayo imethibitishwa “accredited entity”alisisitiza Profesa Kamuzora.

Prof. Kamuzora amesema kuwa huu ni mradi mkubwa sana na wenye manufaa kwa wakazi wa Simiyu ambapo Mfuko wa Mabadiliko ya tabianchi umetoa kiasi cha 102,700,000 EURO, Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW) itachangia 25,900,000 EURO na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itagharamia kiasi cha 13,100,000 EURO. Vilevile jamii inayozunguka mradi itachangia kiasi cha 1,500,000EURO, hivyo mradi wote unatarajiwa kugharimu kiasi cha EURO 143,000,000 na utatekelezwa ndani ya kipindi cha miaka mitano.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Prof. Faustin Kamuzora akifungua mkutano wa wadau wa Utekelezaji wa Mradi wa Maji Simuyu. Mradi huo mkubwa uko katika hatua za mwisho kabla ya kuanza kutekelezwa. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji Eng. Emmanuel Kalobelo.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji Eng. Emmanuel Kalobelo akifunga kikao kazi kilichofanyika katika Ukumbi wa Hazina Mjini Dodoma. Kulia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Prof. Faustin Kamuzora.

Katibu Mkuu Prof. Faustin Kamuzora (watatu kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa kikao kazi wanaohusika na utekelezaji wa Mradi wa maji wa Simiyu mara baada ya ufunguzi wa kikao hicho kilichofanyika katika Ukumbi wa Hazina Mjini Dodoma.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...