Ni simulizi la ukweli linalo husu maisha ya kijana Lugwisha kutoka kitongoji cha Goweko, wilayani Uyui mkoani Tabora ambaye baada ya kumaliza shule ya msingi mnamo mwaka 1994 huko kijijini kwao, alifunga safari hadi jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kutafuta maisha. 


 Miaka kumi baadae kijana Lugwisha akawa amepata mafanikio makubwa yaliyobadilisha maisha yake. Mafanikio katika maisha ya Lugwisha yanasababisha kuinuka kwa maadui ambao hawapendezwi na kufanikiwa kwake. Maadui hawa wanapanga njama mbalimbali za kupambana dhidi ya mafanikio ya Lugwisha. 

Kati ya maadui wa Lugwisha, ni maadui wawili tu ndio wanaonekana kuwa na nia thabiti na ya dhati katika mapambano dhidi ya Lugwisha. Maadui hao ni Beka Msangi pamoja na Bundala. 
Beka Msangi alikuwa mmiliki wa bar iliyo kuwa jirani na bar iliyo milikiwa na Lugwisha. Bar hii ya Lugwisha ilikuwa ni moja kati ya makumi ya vitega uchumi vyake vilivyo muingizia fedha nyingi. Bar ya Lugwisha ilikuwa maarufu sana jijini Dar es Salaam na ilikuwa ikifurika wateja kuanzia Jumatatu hadi Jumapili. 
Bar hii ya Lugwisha ilikuwa katika eneo lenye bar nyingi. Uwepo wa bar ya Lugwisha katika eneo hilo uliua biashara ya karibu bar zote zilizo kuwepo katika eneo ikiwemo bar ya Beka Msangi. Beka Msangi hakutaka kukubaliana na hali hiyo na hivyo kufikia uamuzi wa kusafiri hadi katika kijiji cha Mchukwi wilayani Rufiji mkoani Pwani, kwa ajili ya kumroga Lugwisha. Baada ya kupiga ramli, wachawi wa Rufiji wanaona njia pekee ya kupambana na Lugwisha ni kumuhamisha kichawi yeye na bar yake kwa kutumia uchawi wa Kizigua, ujulikanao kama “Sunkwa”. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...