Taasisi ya Fikra ya Jijini Dar es salaam, ambayo imeamua kujikita katika kuwahamasisha vijana hasa wanaosoma shule za msingi, sekondari na wanafunzi wa vyuo, ikiwa na lengo kuongea nao kuhuhsu changamoto zinazowakabili na kuweza kutambua vipaji vyao, imefanya ziara katika Sekondari Shungibweni ambayo ni ya wasichana iliopo Mkuranga, mkoani Pwani. 

Taasisi hiyo ambayo imezinduliwa hivi karibuni, ilitembelea shule hiyo na kufanya Uzinduzi wake rasmi na baadae kutoa mafunzo mbalimbali kwa wanafuunzi wa shule hiyo.

Ujumbe wa taasisi hiyo ulijumuisha waanzilishi wote wa taasisi hiyo ambao ni
Tarqi Mikidadi Mressa, Kassim Suleman Mketema, Maguli Meja Kapalata, Kennedy Alphonse Mlawa na Ally Mchume. Wanafunzi wa shule hiyo walifurahia ujio huo wa Fikra Foundation katika shule yao.
Sehemu ya Wanafunzi wa shule hiyo wakifatilia kwa makini mafunzo waliyokuwa wakitariwa kutoka kwa ujumbe wa Taasisi ya Fikra.
Picha ya pamoja na Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo.
Mafunzo yakiendelea.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...