TAHMEF
(Tanzania Health and Medical Education Foundation) ni shirika lisilo la
kiserikali (NGO), lililozinduliwa rasmi tarehe 8 Julai 2016 na Naibu
Waziri wa Afya, maendeleo ya jamii, jinsia, watoto na wazee Mhe Dr.
Hamisi Kigwangalla.
Tarehe
8 Julai 2017 TAHMEF ilitimiza mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake, na
katika maadhimisho hayo TAHMEF imetoa huduma bure ya upimaji wa Saratani
ya shingo ya kizazi, wilayani Kondoa, mkoani Dodoma katika viwanja vya hospitali ya Wilaya.
Zoezi
hilo liliendeshwa kwa Muda wa siku mbili (8-9 julai 2017) zaidi ya
wanawake 500 Wilayani kondoa walijiandikisha na kupata huduma bure ya
elimu na upimaji wa saratani ya shingo ya kizazi.
Hivi
sasa TAHMEF inaendesha mradi uitwao NURU YA AFYA unaolenga kuwezesha
wanawake wasio na ajira rasmi na kuendelezwa harakati za kumfikia kila
mtanzania kupitia utoaji wa huduma za afya bure kwa wale wenye kipato
cha chini pia kuchangia vifaa na mahitaji mengineyo ya hospitali katika
vijiji mbalimbali, kuongeza uelewa na ufahamu wa watanzania juu ya
changamoto mbalimbali za afya na jinsi ya kukabili changamoto hizo
mapema.
TAHMEF
inatoa Shukrani za dhati kwa PSI na uongozi wote wa Mkoani Dodoma kwa
ushirikiano mkubwa ulioleta mwitikio mzuri kwa wakazi wa kondoa na
kufanikisha zoezi zima
Wanawake
wakazi wa Kondoa wakipewa elimu juu ya Saratani ya shingo ya kizazi
kabla ya kupewa huduma ya upimaji wa saratani ya shingo ya Kizazi.
Wanawake wakazi wa Kondoa wakisubiri kupewa huduma ya upimaji wa saratani ya shingo ya Kizazi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...