Idara ya Uhamiaji imesema jukumu la Udhibiti wa Uingiaji na Utokaji wa raia
wa kigeni nchini, linatekelezwa kwa mujibu wa Sheria ya Uhamiaji Sura ya 54 (Rejeo la 2016) na wala haiwalengi
wafanyakazi wa Kampuni ya Madini ya Acacia peke yake.
Ni hitajio la kisheria kwa kila raia wa kigeni anayeingia na kutoka nchini kukaguliwa
ili kujiridhisha iwapo hakuna
dosari zozote za Uhamiaji, Ulinzi na Usalama.
Sheria ya Uhamiaji inaitaka
Idara ya Uhamiaji kumhoji mtu yeyote awe raia wa Tanzania au
kigeni bila kujali anafanya kazi kwenye
Kampuni au Shirika gani, pale inapotaka kujiridhisha juu ya
uhalali wa ukaazi wake hapa
nchini na ikijiridhisha kuwa mtu huyu
hana dosari zozote inamwachia huru kama ilivyofanyika kwa wafanyakazi wa Kampuni ya Madini ya Acacia waliohojiwa
na kuruhusiwa kuendelea na safari yao hivi karibuni.
Idara ya Uhamiaji inapenda kuuarifu Umma kuwa hakuna sababu
zozote nje ya matakwa ya Sheria
ya Uhamiaji zinazopelekea Idara
ya Uhamiaji kuweka kizuizi cha kuja au kutoka kwa wafanyakazi wa kigeni wa
Acacia.
Tunapenda kuujulisha Umma
kuwa ni muhimu kwa watanzania na raia wa kigeni wanaokusudia
kuingia na kutoka nchini kuhakikisha wanafuata
Sheria za Uhamiaji ili kutimiza hitajio la kisheria.
Imetolewa
na
Ally M. Mtanda
Msemaji
wa Idara ya Uhamiaji
29
Julai 2017
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...