Idara ya Uhamiaji   imesema jukumu la Udhibiti  wa Uingiaji na Utokaji  wa raia  wa kigeni nchini, linatekelezwa kwa mujibu wa Sheria ya Uhamiaji  Sura ya 54 (Rejeo la 2016) na wala  haiwalengi  wafanyakazi  wa  Kampuni ya Madini ya Acacia  peke yake.

Ni hitajio la kisheria  kwa kila raia wa kigeni  anayeingia na kutoka nchini  kukaguliwa  ili kujiridhisha  iwapo  hakuna  dosari zozote za Uhamiaji, Ulinzi na Usalama.

Sheria ya Uhamiaji inaitaka Idara ya Uhamiaji  kumhoji  mtu yeyote awe raia wa Tanzania au kigeni  bila kujali anafanya  kazi  kwenye Kampuni au Shirika  gani, pale  inapotaka kujiridhisha  juu ya  uhalali  wa ukaazi wake hapa nchini na ikijiridhisha kuwa mtu huyu  hana dosari zozote inamwachia huru kama ilivyofanyika  kwa wafanyakazi wa Kampuni ya Madini ya Acacia  waliohojiwa  na kuruhusiwa kuendelea na safari yao hivi karibuni.

Idara ya Uhamiaji  inapenda kuuarifu Umma kuwa hakuna sababu zozote  nje ya matakwa ya  Sheria  ya Uhamiaji zinazopelekea  Idara ya Uhamiaji   kuweka kizuizi  cha kuja au kutoka kwa wafanyakazi wa kigeni wa Acacia.

Tunapenda kuujulisha Umma kuwa  ni muhimu  kwa watanzania na raia wa kigeni wanaokusudia kuingia na kutoka nchini kuhakikisha wanafuata  Sheria za Uhamiaji  ili  kutimiza hitajio la kisheria.

Imetolewa na
Ally M. Mtanda
Msemaji wa Idara ya Uhamiaji

29 Julai 2017

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...