Na
Veronica Simba – Dodoma
Kufuatia Kongamano
kubwa la Uwekezaji linalotarajiwa kufanyika nchini Uingereza, mwezi Septemba
mwaka huu, Balozi wa Tanzania nchini humo, Dkt. Asha-Rose Migiro amekutana na
wataalam wa Wizara ya Nishati na Madini na Taasisi zake, wakiongozwa na Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo na kujadili fursa za
uwekezaji nchini katika sekta husika.
Katika kikao hicho
kilichofanyika Makao Makuu ya Wizara mjini Dodoma, Julai 24 mwaka huu, Balozi
Migiro, alisema kuwa Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza umejipanga kulitumia
vema kongamano hilo ambapo watanadi fursa za uwekezaji katika sekta zote muhimu
nchini, zikiwemo za nishati na madini.
“Ni kwa sababu hiyo,
nimeona nifike hapa ili nikutane nanyi, tujadili kuhusu fursa za uwekezaji hapa
nchini katika sekta za nishati na madini ili tuweze kuzinadi wakati wa
kongamano hilo,” alisema Balozi Migiro.
Akifungua majadiliano
baina ya wataalam hao na Balozi Migiro, Naibu Katibu Mkuu Pallangyo,
alibainisha kuwa zipo fursa nyingi za uwekezaji hapa nchini, katika sekta za
nishati na madini na kupongeza hatua ya Balozi Migiro kudhamiria kuzinadi fursa
hizo kwa wawekezaji nchini Uingereza.
Aidha, kwa upande wa
sekta ya nishati, Dkt. Pallangyo alimwomba Balozi Migiro kupeleka maombi kwa
Serikali za Uingereza na Ireland kusaidia miradi ya usambazaji umeme vijijini
inayoendelea nchini kote.
Naibu Katibu Mkuu wa
Wizara ya Nishati na Madini, anayeshughulikia masuala ya Nishati, Dkt. Mhandisi
Juliana Pallangyo (kulia) akiwa katika kikao na Balozi wa Tanzania nchini
Uingereza, Dkt. Asha-Rose Migiro (kushoto), Makao Makuu ya Wizara mjini Dodoma
Julai 24, 2017. Wengine pichani ni wataalam wa Wizara na Taasisi zake
walioshiriki kikao hicho.
Naibu Katibu Mkuu wa
Wizara ya Nishati na Madini, anayeshughulikia Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana
Pallangyo (katikati), akiongoza kikao cha wataalam wa Wizara pamoja na Taasisi
zake na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Dkt. Asha Rose Migiro (kushoto kwa
Naibu Katibu Mkuu.)
Balozi wa Tanzania
nchini Uingereza, Dkt. Asha Rose Migiro (mwenye Koti la Pinki) na Naibu Katibu
Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya Nishati, Dkt.
Mhandisi Juliana Pallangyo (kulia kwa Balozi), wakiwa katika picha ya pamoja na
wataalam wa Wizara pamoja na Taasisi zake, Makao Makuu ya Wizara, mjini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu wa
Wizara ya Nishati na Madini, anayeshughulikia Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana
Pallangyo (kulia), akimkabidhi Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Dkt.
Asha-Rose Migiro, Kitabu cha Mpango Kabambe wa Uendelezaji Sekta Ndogo ya Umeme
(Power System Master Plan). Wanaoshuhudia ni wataalam wa Wizara pamoja na
Taasisi zake.
Naibu Katibu Mkuu wa
Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kushoto),
akiagana na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Dkt. Asha-Rose Migiro (kulia),
baada ya kikao baina yao Makao Makuu ya Wizara mjini Dodoma, Julai 24 mwaka
huu.
Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA
Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...