Na Veronica Simba – Dodoma
Kufuatia Kongamano kubwa la Uwekezaji linalotarajiwa kufanyika nchini Uingereza, mwezi Septemba mwaka huu, Balozi wa Tanzania nchini humo, Dkt. Asha-Rose Migiro amekutana na wataalam wa Wizara ya Nishati na Madini na Taasisi zake, wakiongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo na kujadili fursa za uwekezaji nchini katika sekta husika.
Katika kikao hicho kilichofanyika Makao Makuu ya Wizara mjini Dodoma, Julai 24 mwaka huu, Balozi Migiro, alisema kuwa Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza umejipanga kulitumia vema kongamano hilo ambapo watanadi fursa za uwekezaji katika sekta zote muhimu nchini, zikiwemo za nishati na madini.
“Ni kwa sababu hiyo, nimeona nifike hapa ili nikutane nanyi, tujadili kuhusu fursa za uwekezaji hapa nchini katika sekta za nishati na madini ili tuweze kuzinadi wakati wa kongamano hilo,” alisema Balozi Migiro.
Akifungua majadiliano baina ya wataalam hao na Balozi Migiro, Naibu Katibu Mkuu Pallangyo, alibainisha kuwa zipo fursa nyingi za uwekezaji hapa nchini, katika sekta za nishati na madini na kupongeza hatua ya Balozi Migiro kudhamiria kuzinadi fursa hizo kwa wawekezaji nchini Uingereza.
Aidha, kwa upande wa sekta ya nishati, Dkt. Pallangyo alimwomba Balozi Migiro kupeleka maombi kwa Serikali za Uingereza na Ireland kusaidia miradi ya usambazaji umeme vijijini inayoendelea nchini kote.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, anayeshughulikia masuala ya Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kulia) akiwa katika kikao na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Dkt. Asha-Rose Migiro (kushoto), Makao Makuu ya Wizara mjini Dodoma Julai 24, 2017. Wengine pichani ni wataalam wa Wizara na Taasisi zake walioshiriki kikao hicho.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, anayeshughulikia Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (katikati), akiongoza kikao cha wataalam wa Wizara pamoja na Taasisi zake na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Dkt. Asha Rose Migiro (kushoto kwa Naibu Katibu Mkuu.)
 Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Dkt. Asha Rose Migiro (mwenye Koti la Pinki) na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kulia kwa Balozi), wakiwa katika picha ya pamoja na wataalam wa Wizara pamoja na Taasisi zake, Makao Makuu ya Wizara, mjini Dodoma.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, anayeshughulikia Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kulia), akimkabidhi Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Dkt. Asha-Rose Migiro, Kitabu cha Mpango Kabambe wa Uendelezaji Sekta Ndogo ya Umeme (Power System Master Plan). Wanaoshuhudia ni wataalam wa Wizara pamoja na Taasisi zake.
 
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kushoto), akiagana na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Dkt. Asha-Rose Migiro (kulia), baada ya kikao baina yao Makao Makuu ya Wizara mjini Dodoma, Julai 24 mwaka huu.
Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...