Mwanamuziki mkongwe Shaaban Dede amefariki dunia leo saa mbili
asubuhi katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikokuwa amelazwa kwa matibabu
kwa takriban wiki mbili, mwanae Hamad Dede amethibitisha.
Hamad Dede amesema mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwa marehemu Mbagala jijini Dar es salaam, na kwamba ratiba na taratibu zote zitatangazwa mara zitapokamilika kupangwa.
Marehemu Dede atakumbukwa kama mmoja wa wanamuziki nguli kutokea
nchini Tanzania kwa sauti yake tamu na utunzi wa nyimbo mbalimbali zilizoshika
chati akiwa na bendi mbalimbali zikiwemo Tabora Jazz, Bima Lee, Mlimani Park na
Mondo Ngoma ambako alikuwa anatumikia hadi mauti yanamkuta.
Globu ya Jamii inatoa mkono wa rambirambi kwa familia, ndugu, jamaa,
marafiki na mashabiki wa Shaaban Dede
kwa kuondokewa na mkongwe huyu wa muziki.
Mola aiweke roho ya marehemu mahala pema peponi - AMIN
Mola aiweke roho ya marehemu mahala pema peponi - AMIN
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...