Cathbert Kajuna-Kajunason Blog
Mamlaka
ya Mapato Tanzania (TRA) imevifungia vituo zaidi ya 10 jijini Dar es
Salaam kwa kosa la kuendesha biashara bila mashine ya Kielektroniki.
Akizungumza
jijini Dar es Salaam leo wakati wa zoezi la kufungia vituo mbalimbali,
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Charles Edward
Kichere amesema kuwa kwa sasa zoezi hilo linaendelea nchi nzima ili
kuumbua vituo vyote vinavyokwepa kulipa kodi.
"Tuliwapa
muda wafunge mashine hizo mpaka mwaka jana 2016 mwishoni lakini mpaka
sasa hawajatekeleza agizo hilo hivyo hatuna budi kuvifunga hivyo vituo
mpaka pale watakapotekeleza matakwa ya serikali," amesema Kamshna
Kichere.
Kwa
upande wa Kamishna wa Mapato ya ndani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania
(TRA), Bw. Elijah Mwandumbya amesema wakati umefika kwa wafanyabiashara
kufuata makubaliano wanayokuwa wakiwafanya na TRA ili kuepuka usumbufu
unaojitokeza kwa sasa.
Ameongeza kuwa sheria kali zitachukuliwa kwa wafanyabiashara wote ambao
vituo vyao vya mafuta vimefungwa na wakakaidi.
Kamishna
Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Charles Edward Kichere
(mwenye miwani kulia) akimuhoji msimamizi wa kituo cha GBP cha Sinza
Mori jijini Dar es Salaam mara baada ya kufika kwa ajili ya zoezi la
kukifungia kituo hicho kwa kukosa kuwa na mashine za kielektroniki.
Wengine ni wafanyakazi wa TRA walioambatana nae.
Kamishna
Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Charles Edward Kichere
(aliyenyoosha mkono) akiwahimiza vijana wake wafunge kituo hicho.
Kamishna
Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Charles Edward Kichere
(kushoto) akiwa na Kamishna wa Mapato ya ndani wa Mamlaka ya Mapato
Tanzania (TRA), Bw. Elijah Mwandumbya (kulia) wakitoa msisitizo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...