NA EVELYN MKOKOI.
NAIBU Waziri Ofisi ya Makamu wa
Rais Muungano na Mazingira Luhaga Mpina ,amesitisha uchimbaji na
uchotaji wa mchanga kiholela katika maeneo yasiyo rasmi.
Pia ametoa siku 30 kwa Halmashauri za Manispaa za Jiji la Dar es Salaam kubaini na kutenga maeneo ya uchimbaji ya mchanga ambayo yapo ndani ya manispaa zao yatakayo ruhusiwa kwa zoezi hilo kisheria.
Pia ametoa siku 30 kwa Halmashauri za Manispaa za Jiji la Dar es Salaam kubaini na kutenga maeneo ya uchimbaji ya mchanga ambayo yapo ndani ya manispaa zao yatakayo ruhusiwa kwa zoezi hilo kisheria.
Akitoa agizo hilo Dar es Salaan
leo,wakati wa ziara ya kutembelea Mto Nyakasangwe uliopo maeneo ya Boko
Kata ya Bunju alisema kama kuna maeneo ambayo wananchi wanaweza kufika
Kwa urahisi, manispaa zinapaswa kuyatembelea maeneo hayo na kuyabaini
kama kunauwezekano wakuchimba mchanga.
Alisema ndani ya mwezi mmoja
manispaa hizo zinatakiwa kuandaa utaratibu mfupi wa kutenga maeneo hayo
ikiwemo utoaji wa vibali kutoka Wizara ya Nishati na Madini,Halmashauri
pamoja na Nemc.
“Halmashauri zote zilizo na eneo
ambalo linaweza kuruhusiwa kuchota mchanga hakikisheni mnatembelea
maeneo hayo na kufata taratibu zote za utoaji wa vibali ambapo maeneo
mengine yawe ya uchotaji wa mchanga,”alisisitiza Mpina
Eneo la mto Nyakasangwe lililopo kaika kata ya Bunju linavyoonekana kuharibika vibaya kutokana na uchimbaji wa mchanga , na kupelekea makazi ya wananchi kuwa hatarini.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akizungumza na vyombo vya habari baada ya kukamilika kwa zoezi la kukagua mto Nyakasangwe, uliopo katika kata ya Bunju ulioharibiwa vibaya na uchimbaji wa mchanga.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akimsikiliza Mwandishi wa Habari wa kituo cha Radio cha Efm kinachopatikana katika masafa ya 93.7 katika jiji la Dar es Saalam alipokuwa akimuuliza maswali kuhusu uchafuuzi wa mazingira utokanao na uchimbaji wa mchanga katika eneo la Boko.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...