Tumepata taarifa kwamba kuna matapeli wamekuwa wakiwahadaa wanafunzi wanaoomba udahili wa mwaka wa kwanza Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kuwapa taratibu zisizo sahihi na kisha kuwaibia fedha zao.
Tunaomba kuujulisha umma kwa ujumla kwamba udahili Chuo Kikuu cha Dar es Salaam unafanywa kwa kupitia mfumo wa kompyuta katika mtandao maalumu unaopatikana katika tovuti iliyopo kwenye anuani: udsm.admission.ac.tz. Maelezo ya jinsi ya kuomba udahili pamoja na habari nyingine za udahili zinapatikana katika tovuti ya chuo yenye anuani: www.udsm.ac.tz.
Maombi hayapokelewi kwa kujaza fomu. Pili, ada ya maombi ya udahili ni Shilingi 20,000/= tu ambazo zinalipwa kwa kutumia mitandao ya simu kwa kufuata maelekezo yaliyowekwa kwenye mfumo wa udahili.
Tunatoa pole kwa waliopata usumbufu na tunasisitiza umuhimu wa kufuata taratibu zilizo rasmi katika zoezi zima la udahili.

Tunawatakia udahili mwema.

Imetolewa na Kurugenzi ya Shahada za Awali
Simu:       +255222410069

+255222410751

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...