Tunapenda kutoa taarifa kwa Ndugu, Jamaa, Marafiki, Familia na wote tuliopatwa na msiba huu wa marehemu Professor Henslay William Kabisama uliyotokea huko Ontario, California, Marekani.
Mwili wa mpendwa wetu Prof Henslay Kabisama umewasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam jana Ijumaa Julai 21, 2017 saa tisa mchana. Tunaombeleza nyumbani kwa marehemu Ursino Victoria nyuma ya Ofisi za Halotel.
Mazishi yatafanyika leo Jumamosi Julai 22, 2017 yakitanguliwa na Ibada ambayo itafanyika katika kanisa la St. Alban Upanga saa saba kamili mchana. Baada ya hapo tutaelekea makaburi ya Kinondoni kwa mazishi.
Bwana alitoa na bwana ametwaa
Jina la Bwana libarikiwe
AMEN.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...